Dr.Jakaya Mrisho Kikwete alipowahutubia katika ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es Salaam leo mchana(Picha na Freddy Maro)
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Oct 9, 2010
Rais Kikwete aongea na wana CCM Wilaya ya Ilala!
MAMA SALMA KIKWETE AONYA WANAOFANYA KAMPENI KWA KUTUMIA UKABILA NA UDINI!!
MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amesema kufanya kampeni kwa kutumia udini na ukabila ni kuhatarisha amani.
Alisema hayo juzi na jana alipozungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoani hapa, alipokuwa akiwaombea kura wagombea wa Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Mama Salma alisema kuwagawa Watanzania kwa misingi ya udini na ukabila ni kutaka kutowesha amani ambayo imedumu nchini kwa miaka mingi.
“Udini na ukabila utatutenganisha, tutahasimiana kwa sababu huyu ni mkristo na yule ni muislamu, haya ni yale yale ya huyu ni Mtutsi na yule ni Mhutu, jamani kina mama huko ndiko tunataka kwenda ?” Alihoji na kujibiwa “hapana”.
Mama Salma alisema, wanachama wa vyama vya siasa wana dini zao, lakini usajili wa vyama hivyo haufanyiki kwa kuangalia dini na kabila, hivyo kufanya kampeni kwa vigezo hivyo ni ukiukaji wa sheria.
Wakati akizungumzia hilo, kina mama hao walikuwa wakimwitikia kwa kusema “sema mama usiogope” kuashiria kuna baadhi ya watu wanafanya kampeni za kibaguzi kwa kutumia udini na ukabila.
Mwenyekiti huyo wa WAMA ambaye ni mke wa mgombea urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, alitahadharisha kwamba, amani kuvunjika ni rahisi, kuirejesha ni kazi kubwa na mifano ipo katika baadhi ya nchi za Afrika ambazo ziliichezea na haijarejea.
Aliwaambia wananchi wa Kigoma kwamba wao ni mashahidi wa namna nchi jirani zilivyoathirika kutokana na machafuko chanzo kikiwa ni siasa za kibaguzi zilizojiegemeza kwenye udini na ukabila.
Mama Salma aliwaombea kura wagombea ubunge kwa tiketi ya CCM; Injinia Christopher Chiza (Buyungu), Jamal Tamimu (Muhambwe), Daniel Nsanzugwanko (Kasulu Vijijini), Raphael Neka (Kasulu Mjini), Robson Lembo (Kigoma Kaskazini), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Gulamuhussein Kifu (Kigoma Kusini).
Diamond Kutua UK November 2010!
Jakaya Kikwete atimiza miaka 60 ya kuzaliwa kwake!!
JAJI MFAWIDHI ERNEST MWAIPOPO AAGWA RASMI LEO JIJINI DAR ES SALAAM!!
Jaji Mfawidhi wa Divisheni ya Mahakama ya Kazi ya Mahakama Kuu, Ernest Mwaipopo akizungumza na majaji,mawakili , wageni waalikwa na wadau mbalimbali wa sheria wakati wa hafla ya kumuaga rasmi kitaaluma iliyofanyika mahakama kuu leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine ametoa wito wa kufanyika kwa utaratibu wa shughuli za mahakama zikiwemo uandikaji wa hukumu na mienendo ya kesi kutumia lugha ya kiswahili ambayo inatumiwa na kueleweka miongoni mwa wananchi.
MSIMAMO WA WAHARIRI WA HABARI ZA MICHEZO KUHUSU UINGIAJI MECHI YA STARS V MOROCCO
LEO Ijumaa Oktoba 8, wahariri 37 wa habari za michezo kutoka vyombo mbalimbali vya habari walikutana mgahawa wa Hadee’s jijini Dar es Salaam kuzungumzia masuala ya uingiaji wa waandishi wa habari kwenye mchezo wa kesho kati ya Taifa Stars na Morocco.
Kama tunavyofahamu ni kuwa TFF imetangaza kwamba itatoa tiketi maalum mchezo wa Taifa Stars na Morocco, badala ya kadi ambazo zimekuwa zikitumika katika michezo mbalimbali ya ligi.
Kutokana na malalamiko ambayo yamekuwa yakitolewa na wanahabari za michezo kupinga uamuzi huo wa TFF, Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kiliitisha mkutano na wahariri wa habari za michezo.
Mambo mbalimbali yalizungumzwa, huku malalamiko yakiwa mengi kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linawanyanyasa waandishi wa habari na kuwatumia pale tu linapokuwa na maslahi yake.
Msimamo wa kikao ni kuwa kadi za TFF zinazotumika kwenye michezo mbalimbali si nyingi kama wengi wanavyodhania, na kwamba ingawa TFF inasema ilitoa kadi 170 mwaka 2008, idadi halisi ya wanaofanya kazi hiyo hawafikii hata 100.
Kwa misingi hiyo wajumbe wa kikao walikubaliana kwamba TFF itamke kuwa waandishi wa habari za michezo waruhusiwe kutumia kadi hizo kwa sababu wapo wanaoenda kwenye mechi kwa ajili ya kuripoti mpira, wengine kuandika makala, wengine kupiga picha na wengine matukio ya kawaida yasiyohusiana na mchezo wa uwanjani.
Mjumbe mwalikwa wa kikao hicho, Florian Kaijage ambaye ni Ofisa Habari wa TFF, alipopewa nafasi ya kuzungumza aliwaeleza wahariri kuwa tayari utaratibu uliokuwa umepangwa ni kuwa hakuna atakayepita mlangoni bila kuwa na tiketi.
Hivyo aliwaeleza wajumbe hata kama watakubaliana zitumike kadi, italeta vurugu kwenye majukwaa kwa sababu tiketi zina namba za viti.
Kaijage alipewa fursa ya kusikiliza hoja mbalimbali na mwishoni aliombwa na kikao aendelee na shughuli zake, lakini msimamo ukiwa wahariri wanataka zitumike kadi na si vinginevyo.
Hata hivyo baada ya majadiliano ya muda mrefu, kujali utaifa pamoja na busara za kiuhariri tulikubaliana yafuatayo:
- Kwa kuwa TASWA na Wahariri wanaamini TFF imekuwa ikifaidika zaidi na vyombo vya habari kwa kuandikiwa habari zao nyingi ambazo nyingine ni promosheni, kuna haja ikawathamini katika hili.
TASWA na Wahariri wanaamini kwa kuwa idadi ya waandishi wanakaoingia uwanjani ni chache tofauti na wengi wanavyofikiri, na pia wengi wa waliopewa kadi mwaka 2008 hivi sasa karibu 50 hawapo kwenye vyombo vya habari na TFF haina haja ya kuogopa hilo.
- Lakini kwa sababu TFF inasema ukaaji uwanjani utahusu namba za viti, basi TFF itenge tiketi 120 kwa ajili ya wanahabari.
Tiketi hizo zitasimamiwa na Ofisa Habari wa TFF kwa kushirikiana wa Wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji ya TASWA, ambao ni Mhazini Sultani Sikilo na Mjumbe Grace Hoka.
Hawa watazigawa tiketi hizo kwa wote watakaokuwa na kadi za TFF za kuingia uwanjani zilizotolewa mwaka 2008.
Hivyo kitakachofanyika ni kwa mhusika kuonesha kadi yake ya TFF atapewa tiketi ya Taifa Stars na Morocco ili aingie uwanjani.
Hili litasaidia pia kudhibiti wale ambao hawapo kwenye vyombo vya habari, lakini wanamiliki vitambulisho, pia kuwa na uhakika wa namba halisi ya wenye vitambulisho badala ya hiyo ya TFF ambayo inaonekana si sahihi.
Hivyo kama hilo litakubaliwa waandishi wa habari za michezo wataombwa kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa 6 mchama wafike ofisi za TFF Uwanja wa Karume, Dar es Salaam ili wapewe tiketi lakini kwanza waoneshe hizo kadi za TFF.
(4)Viongozi wa TASWA wawasiliane na TFF wawaeleze msimamo huu na kama itatokea wenye kadi wakazidi idadi ya tiketi, hilo litafanyiwa kazi na busara itatumika kati ya TASWA na TFF ili kila anayestahili aweze kufika uwanjani.
Hata hivyo angalizo la wahariri ni kuwa wale ambao wanaelewa hawapo kwenye vyombo vya habari kwa sasa, hata kama wanazo kadi za kuingia uwanjani, wasiende maana hawatapewa tiketi na badala yake kadi zao zitazuiwa.
MSIMAMO:
Kama TFF ikishindwa kutekeleza hayo mapendekezo basi yafuatayo yatafanyika:
(1)Tiketi 70 ilizopanga TFF kutoa kwa ajili ya wanahabari hazitachukuliwa na mwandishi yeyote, badala yake TFF wazitumie wenyewe kadri watakavyoona inafaa wenyewe.
(2)Vyombo vya habari vigharamie watu wake kwenda kuripoti mechi hiyo, bila kujihusisha kwa namna yoyote na TFF.
(3)Waandishi wa habari hawatajihusisha na kuandika habari za TFF zinahusu promosheni ya aina yoyote, isipokuwa habari ambazo ni za maslahi kwa Taifa ikiwemo mechi za timu za Taifa.
Lakini masuala mengine ya TFF, ikiwemo kutangaza viingilio, adhabu za waamuzi ama hata kupata udhamini wa kitu fulani, wahariri wamekubaliana kwamba hilo halitafanywa.
Pia hata upigaji picha viwanjani katika maeneo ambayo ni kuitangaza TFF hayo hayatapewa nafasi.
Masuala mengine muhimu juu ya nini kifanyike wahariri wamekubaliana tena wakutane Jumatano wiki ijayo kujadili tena mambo mengine ya kufanya, ikiwa ni pamoja na utaratibu mzuri wa waandishi kuingia uwanjani na kufanya kazi zao bila bugudha.
Karibu vyombo vyote vya habari vilishiriki kwenye mkutano huo, ambao wengi waliupongeza uongozi wa TASWA kwamba ni mwanzo mzuri.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
08/10/2010
TFF REKEBISHENI HILI KWA MANUFAA YA JAMII KUPATA HABARI!!
MATAIFA YA AFRIKA YAHIMIZWA KUJIUNGA NA SEAMIC KUENDELEZA MADINI!!
MATAIFA ya Bara la Afrika yametakiwa kujiunga na Kituo cha Utafiti na Uendelezaji wa Sekta ya Madini Kusini na Mashariki mwa Afrika(SEAMIC) ili kuhimili mahitaji yaliyopo katika sekta ya madini katika nchi zao.
Hayo yamesema leo na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakati alipokuwa akipokea hati ya utambulisho ya uanachama wa Sudani katika SEAMIC Jijini Dar-Es-Salaam.
Waziri Ngeleja alisema mataifa ya Afrika yamekuwa yakitumia gharama kubwa ya rasilimali fedha katika usafirishaji wa sampuli za madini kwa ajili ya utafiti wa kimaabara katika nchi za nje pasipo na kuitumia fursa ya SEAMIC, ambayo imeweka wazi dhamira yake katika kuongeza ufanisi wa shughuli za madini.
Kwa mujibu wa Waziri Ngeleja anasema tangu SEAMIC ianze shughuli zake hapa nchini mwaka 1997, Tanzania imeweza kufanya utafiti wa sampuli 35000 za madini, na hivyo kulifanya taifa kuokoa kiasi kikubwa cha fedha za usafirishaji wa sampuli hizo nje ya nchi..
“Kama tutakuwa na wanachama wengi wa SEAMIC itasaidia mataifa yetu ya Afrika kumudu changamoto mbalimbali katika sekta ya madini ikiwemo rasilimali fedha na kuongeza ufanisi, hivyo ni wito kwa mataifa yote kushirikiana nao kwa kuzingatia kuwa mwanachama anaweza kujiunga kwa wakati wowote”.
Aidha Waziri Ngeleja alisema SEAMIC pamoja na majukumu mengine imedhamiria kuongeza maarifa katika usimamizi wa madini, kubadilisha takwimu za madini, kuongeza ubora wa madini na kufanya utafiti wa kimaabara kwa sampuli mbalimbali za madini.
Waziri Ngeleja anaongeza kuwa SEAMIC pia imeeleza nguvu zake katika kusaidia wazalishaji wadogo wa madini katika maeneo mbalimbali, ili kuhakikisha kuwa wachimbaji hao wananufaika na shughuli hizo zinawaongezea tija na ufanisi mkubwa zaidi.
Naye Balozi wa Sudan hapa nchini, Abdel-Bagi H. Kabeir anasema, Serikali yake itatumia vyema fursa ya uanachama wa SEAMIC kwa kuzingatia maslahi ya wananchi wote wa Sudan na Bara la Afrika kwa ujumla wake, kwani nchi hiyo imebahatika kuwa na rasilimali nyingi katika sekta ya madini na nishati.
Tumejiandaa kikamilifu katika kuhakikisha kuwa fursa ya uanachama huu inatumika kikamilifu katika nchi yetu na hilo litaweza kuonekana katika kipindi kifupi kijacho” anasema Balozi Kabeir
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa SEAMIC, Bw. Katema Tadesse anasema tangu taasisi hiyo iingie nchini jumla ya wachimbaji wadogo 500 wameweza kupewa mafunzo katika namna ya kuendesha shughuli za madini, ikiwemo kutafuta masoko na kuongeza thamani ya madini katika maeneo yao ya uzalishaji.
Tadesse anasema uanachama wa SEAMIC upo wazi kwa kila nchi za Afrika, hivyo kutoa fursa hiyo ina yenye manufaa kwa kuwa shughuli zake zitasaidia mataifa katika nyanja mbalimbali ikiwemo mafunzo, uzalishaji, uchimbaji wenye kuzingatia utunzaji wa mazingira, utafiti wa kimaabara wa sampuli za madini.
DK. GHALIB BILAL AKIWA KITETO JANA!!
Oct 7, 2010
Katibu Mkuu Habari akemea vyombo vya habari vinavyoandika habari za uchochezi!!
Serikali imeonya vyombo vya habari kuacha mara moja kuandika habari za uchochezi unaolenga kuwachonganisha wananchi na Serikali yao iliyopo madarakani.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Bw.Sethi Kamuhanda wakati mkutano wake na wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Tanzania(TSN) kwenye ziara yake ya siku moja kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali zinazoendeshwa na kampuni hiyo.
Alisema kuwa ni vema vyombo vya habari vikafanya kazi hapa nchini kutoa habari zinazozingatia weledi wa taaluma ya uandishi wa habari na sio kupandikiza uchochezi miongoni mwa Watanzania na hivyo kuzorotesha amani.
Kamuhanda alisema kuwa Serikali haitavumilia hali ya uchochezi inayofanywa na baadhi ya vyombo vya habari vinavyomilikiwa wageni na vile vya ndani vinavyopandikiza chuki na kuichafua Tanzania.
"Tunaomba vyombo vya habari vyote ambavyo vimefanya uchochezi kuwa sehemu ya professional kuacha mara moja kwani wakitulazimisha tuvifungia au kufuta katika usajili ...tunawaomba kuandika habari ambazo hazina uchochezi na zinazozingatia taratibu na Sheria zilzopo" alisisitiza Katibu Mkuu huyo.
Alisema kuwa pamoja na uhuru uliopo kwa vyombo vya habari nchini ni vema wakautumia vizuri badala ya kugeuza vyombo vya habari kuwa uwanja wa uchochezi unaotishia amani.
Kamuhanda alitoa mfano kuwa kuwa baadhi ya Nchi zijikuta katika machafuko na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu ya vyombo vya habari vilivyofanya uchochezi kuwa kama ajenda yao kubwa na kuongeza kuwa Serikali halifumbia macho chombo cha habari chenye mlengo huo.
Hata hivyo alisema Serikali itaendelea kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari na kusajili vingine vingi ili cha msingi kwa waandishi wa habari ni kuzingatia weledi wa uandishi wa habari ili uhuru huo ulete maana halisi.
Kwa upande wa wananchi walitoa maoni yao kuhusu agizo hilo la Katibu Mkuu walisema kuwa tamko hilo ni vema likaanza kutekelezwa kwani wamechochosa na baadhi ya vyombo vya habari kugeuzwa majukwaa ya kupandikiza chuki katik ya kundi moja na lingine.
WAZIRI MKUU AZINDUA MRADI WA MATREKTA LUGALO
TAMKO LA KAMATI YA UTENDAJI YA TASWA KUHUSU UINGIAJI UWANJANI MECHI YA MOROCCO V TAIFA STARS
CHAMA Cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kimesikitishwa na hatua ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza itatoa tiketi kwenye mechi ya Taifa Stars na Morocco badala ya kadi ambazo zimekuwa zikitumika karibu kila mechi kubwa.
Hatua hii ya TFF tunaiona kama ni ubaguzi na pia kutaka kuwagawa waandishi wa habari za michezo maana walio wengi watakosa kwenda kushuhudia mchezo huu, licha ya juhudi kubwa walizofanya katika kuutangaza kwa umma.
TASWA hailazimishi waandishi wa habari waingie wote, lakini inasikitishwa na namna wanavyonyanyaswa hasa linapokuja suala la mechi kubwa zinazofanyika Uwanja Taifa Dar es Salaam.
Sote tunakumbuka tukio la Juni mwaka huu wakati wa mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Taifa Stars na Brazil ambayo waandishi walio wengi walishindwa kuingia uwanjani kutokana na utaratibu ambao haukuwa mzuri, na ulioleta malalamiko kwa wanachama wetu.
Kwa kutambua hili uongozi mpya wa TASWA ulipoingia madarakani Agosti 15 mwaka huu, siku mbili baadaye yaani Agosti 17 Siku ya Jumanne saa tano asubuhi, ujumbe wa viongozi watatu wa juu wa TASWA ulienda ofisi za TFF Uwanja wa Karume Dar es Salaam kujitambulisha na pia kuzungumza masuala mbalimbali yahusiyo waandishi wa michezo na namna ya kuingia uwanjani.
Upande wa TASWA waliohudhuria walikuwa ni Mwenyekiti, Juma Pinto, Makamu Mwenyekiti, Maulid Kitenge na Katibu Mkuu, Amir Mhando, wakati upande wa TFF uliwakilishwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Athumani Nyamlani, Kaimu Katibu Mkuu, Sunday Kayuni, Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage na Wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji, Eliud Mvella na Muhsin Said.
Ikumbukwe kikao hiki kilifanyika siku moja kabla ya mchezo wa Ngao ya Hisani kati ya Simba na Yanga, hivyo tulijadiliana kwa kirefu namna ya waandishi kuingia uwanjani hasa tukirejea tukio la mechi ya Stars na Brazil.
Kwenye mjadala huo tulikubaliana kwamba wakati utaratibu mwingine ukiandaliwa ambao utaridhiwa na pande zote mbili yaani TASWA kama wawakilishi wa waandishi wa habari za michezo na TFF kama wasimamizi wa mpira nchini, zitumike kadi ambazo TFF ilizitoa miaka miwili iliyopita kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, ili kuepusha usumbufu kwani zinatumika kwenye ligi.
Tulifikia uamuzi huo wa kutumia kadi kwa kuwa TFF ndiyo iliyozitoa na si nyingi kama wengi wanavyofikiria, mjadala ulikuwa mbona mechi nyingine huwa zinatumika? Hivyo kikao kikaazimia kwamba zitumike kadi hizo na hilo likafanyika na limekuwa likifanyika.
Mambo mengine ikiwemo suala la ukaaji wa waandishi wa habari uwanjani lilizungumzwa lakini ikaonekana kwa Uwanja wa Uhuru TFF wakasema hawana mamlaka nalo, lakini tukapeana muda wa kulitafutia ufumbuzi.
Hili la namna ya ukaaji uwanjani napenda tuseme wakati TASWA mpya ilipoenda kujitambulisha kwa Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo na aliahidi kwamba kwa kushirikiana na TFF watalifanyia kazi.Hivyo hatuna wasiwasi nalo.
Lakini TASWA imesikitishwa sana na kauli iliyotolewa na uongozi wa TFF kwamba watatoa tiketi badala ya zile kadi zao ambazo ndizo waandishi wanatumia iwe mechi ya Stars au timu nyingine yoyote maana kwetu tuliona ndizo 'ACCREDITATION' za TFF viwanjani.
Tunashangaa kwamba TFF kwa makusudi imeamua kuyaweka kapuni yale tuliyozungumza kwenye kikao cha Agosti 17 na kwa kweli hili ni jambo ambalo halipaswi kufanywa na watu wanaofanya kazi kwa pamoja, sisi tukiwa wadau wakubwa wa TFF.
Tunachokiona hapa TFF ina huruma ya mamba, ambaye anakutafuna huku anatoa machozi ukidhani kwamba anakuonea huruma kumbe ndiyo staili yake ya kukumaliza.
Kwa msingi huo Taswa haipo tayari na haikubaliani na utaratibu wa utoaji kadi uliotangazwa na TFF badala yake tunasisitiza umuhimu wa kutumika zile kadi ambazo zinatumika kwenye mechi mbalimbali.
Tunajiuliza maswali kwa nini Morocco? Kwa nini waandishi waelezwe mabadiliko sasa? TFF ina nini? Mbona haikutujulisha kwamba siku tunajadili kwenye kikao ilikuwa tunapoteza muda?
Kwa misingi hiyo tunaandaa mkutano wa pamoja kati ya Taswa na wahariri wa michezo wa vyombo mbalimbali vya habari kesho ili tutoke na msimamo wa pamoja kuhusu TFF na hatua gani tuchukue kutokana na mambo haya ya waandishi wa michezo kutothaminiwa.
Tunawasisitiza wanachama wa Taswa waendelee kuwa watulivu kipindi hiki wakati tukitafuta ufumbuzi wa jambo hilo, lakini kwa kuanzia TASWA haikubaliani na utaratibu huu, hivyo TFF waufanye wenyewe kwa sababu wao ndio wenye mamlaka ya mpira na wanaona hatuna la kufanya na mawazo yetu huwa yanapuuzwa, kwani wametuomba tushirikiane nao kuandaa uataratibu wa tiketi hizo lakini hatutajiingiza huko maana kama hawakuheshimu kikao cha Agosti 17 itakuwa leo?
Hata kama TASWA itatoa mawazo mazuri namna gani, TFF haiwezi kuyafanyia kazi.Waendelee wenyewe na utaratibu wao maana kusudi haina pole.
Chama kimekuwa kikipokea shutuma nyingi kwa uamuzi unaotolewa na TFF sisi hatutaki tuwe kama yale mambo ya msafara wa ng’ombe, ambaye anayechelewesha yuko mbele,lakini viboko anapigwa wa nyuma ambaye ni TASWA. Hilo hatutalikubali hata kidogo.
Tunaishauri TFF iwe makini na jambo hili, vinginevyo heshima ya shirikisho hilo itaingia matundu bila sababu za msingi ni kama watu waliojificha mvua kwenye mpapai.
Tunamalizia kwa kusema kuwa kama TFF wenzetu wanajua mbio, sisi tunaelewa njia
Ahsanteni
katibu mkuu taswa
SERENGETI YAIMWAGIA CECAFA MILIONI 675!
morocco ndani ya dar
Oct 6, 2010
MIKUTANO YA MWAKA YA SHIRIKA LA FEDHA LA KIMATAIFA NA KUNDI LA BENKI YA DUNIA YAANZA.
Mikutano ya mwaka ya Bodi ya Magavana ya Shirika la fedha la Kimataifa na kundi la Benkiya Dunia kwa mwaka 2010 imeanza leo mjini Washington D.C. Kilele cha mikutano hiyo kitakuwa tarehe 8 - 10, mwezi Octoba 2010.
Bodi ya Magavana wa Shirika la Fedha la kimataifa ( Mfuko) na Bodi ya Magavana wa kundi la Benki ( Benki ) kwa kawaida hukutana mara moja kwa mwaka kujadili kazi za Taasisi zinazowahusu. Mikutano hii ya mwaka huwa inafanyika mwezi Septemba hadi Octoba, hufanyika mjini Washington kwa miaka miwili mfululizo na kwa mwaka wa tatu hufanyika kwa nchi mwanachama.
Uzinduzi wa Mikutano hii ya Bodi ya Magavana ulifanyika Savannah, Georgia, Amerika mwezi Machi mwaka 1946. Na mikutano ya kwanza ya mwaka ilifanyika mjini Washington mwaka1946.
Mwaka huu,Mikutano ya mwaka itaambatana pamoja na mikutano ya kimataifa ya kifedha na kamati za fedha, Kamati za maendeleo, kundi la nchi kumi, kundi la nchi ishirini na nne, na makundi mbalimbali ya nchi wanachama.
Aidha mwisho wa mikutano hii, Shirika la fedha la kimataifa, kamati ya mambo ya fedha, Kamati ya maendeleo pamoja na makundi mengine watapata nafasi ya kuwasiliana na kutoa mapendekezo yao.
Mikutano hii ya mwaka itaunganisha siku za utangulizi kabla ya ufunguzi rasmi kipindi ambacho Magavana watakitumia kwa kuzungumzia masuala ya kibiashara na kushauriana.Vilevile katika Mikutano hii ya mwaka, Bodi ya Magavana huwa inafanya maamuzi ya ni vipi mambo ya Fedha ya kimataifa yanapaswa kuwa na kukubaliana kuhusu maazimio husika.
Mikutanoya mwaka inakuwa na mwenyekiti ambaye ni Gavana wa Benki na wa Mfuko, na uenyekiti huo unakuwa ni wa kupokezana kati ya wanachama kila mwaka. Kila baada ya miaka miwili inachagua Mkurugenzi mtendaji. Kila mwaka wanachama wapya wowote wanakaribishwa katika Benki na mfuko.
Kwa sababu Mikutano hii ya mwaka inakusanya idadi kubwa ya wanachama kutoka nchi mbalimbali, hivyo shirika la fedha la kimataifa na kundi la Benki ya Dunia inatoa nafasi ya kuwapatia ushauri mkubwa na mdogo, kwa mpangilio wa kuwa na utaratibu maalumu au kutokuwa na utaratibu maalumu alimradi hawavurugi mpangilio uliopo.
Semina mbali mbali zinafanyika wakati wa mikutano na zinaaendeshwa na wafanyakazi wanachama kwa waandishi wa habari.Programu za Mikutano ya mwaka zimetengenezwa kwa kuzingatia matakwa ya sekta binafsi, wajumbe kutoka Serikalini na maafisa wakuu wa Mabenki na watumishi wa Mfuko.
Mikutano ya mwaka nje ya Amerika kuanzia mwaka
1947--2009
Mwaka | Nchi |
1947 | London |
1950 | Paris |
1952 | Mexico City |
1955 | Istanbul |
1958 | New Delhi |
1961 | Vienna |
1964 | Tokyo |
1967 | Rio de Janeiro |
1970 | Copenhagen |
1973 | Nairobi |
1976 | Manila |
1979 | Belgrade |
1982 | Toronto |
1985 | Seoul |
1988 | Berlin |
1991 | Bangkok |
1994 | Madrid |
1997 | Hong Kong |
2000 | Prague |
2003 | Dubai |
2006 | Singapore |
2009 | Istanbul |
Magavana wa mikutano hiyo ni Mawaziri wa fedha kutoka nchi mbalimbali, Magavana wa Benki kuu na Makatibu wa kuu wa Wizara za fedha.
Mpaka sasa karibu nchi zote zimeisha wasili katika mikutano hiyo.
Imetolewa na:
Ingiahedi Mduma
Msemaji Mkuu
Wizara ya Fedha na uchumi
Washington D.C