Oct 7, 2010

SERENGETI YAIMWAGIA CECAFA MILIONI 675!

Katibu Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye kushoto akipokea Mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 675 kutoka kwa Mkurungenzi Mkuu wa SBL Ajay Mehta kulia ni Caroline Ndungu Mkurugenzi wa Masoko SBL na katikati ni Meneja Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano SBL Teddy Mapunda. Kampuni ya bia ya serengeti ISBL) kupitiam bia yake ya Tusker itadhamini mashindano hayo kwa jumla ya shilingi miloni 675 za kitanzania kwa ajili ya kuendesha mashindano hayo ikiwa ni pamoja na kugharamia tiketi za ndege kwa timu shiriki na maafisa wa CECAFA pamoja na marefa, malazi, usafiri wa ndani, uratibu, zawadi, ada mbalimbali, usalama, gharama za kutumia uwanja, usajili wa waandishi wa habari na gharama nyinginezo. Michuano hiyo inatarajiwa kuanza tarehe 27 Novemba mpaka tarehe 11 Disemba mwaka huu ambapo mashindano hayo yanafanyika hapa nchini kwa mwaka huu. Maswhindano ya CECAFA mwaka huu yatashirikisha timu kutoka Kenya, Uganda, Rwanda, Burubdi, Djibouti, Somalia, Ethiopia, Sudan, Tanzania, Zanzibar Eritrea na kwa mara ya kwanza CECAFA imeialika timu ya Ivory Coast kama timu mwalikwa wa mashindano hayo. SBL ndiyo mdhamini mkuu wa mashindano hayo ya CECAFA 2010 kupitia kinywaji chake cha TUSKER
Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye, Mkurugenzi wa Masoko SBL Caroline Ndungu na Teddy Mapunda Meneja Uhusiano na Mwasiliano SBL.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA