Aliyekuwa msemaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF Frolian Kaijage kushoto akiongea na Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari TASWA Juma Pinto hivi karibuni kabla ya kupigwa chini na TFF.
Shirikisho la soka nchini TFF limemsimamisha kazi msemaji wa Shirikisho hilo TFF FROLINAN KAIJAGE baada ya kushindwa kupiga nyimbo za taifa wakati wa mchezo wa kufuzu fainali za mataifa la Mataifa ya afrika kati ya morocco na Taifa Stars ya Tanzania.
Kabla ya kuanza kwa mchezo huo ambapo rais kikwete alikuwa mgeni rasmi baada ya kukagua timu Rais alisubiri kwa muda ili nyimbo za mataifa yote mawili kupigwa kama ilivyo kawaida, lakini hakuna kilichosikika zaidi mashabiki wa timu ya Taifa Stars ambao walianza kuimba wimbo huo wakisikika "mungu ibariki yanga".
Mpaka sasa bado haijafahamika kwanini nyimbo hizo zilishindwa kupigwa na kufuatia kitendo hicho TFF imeamua kumsimamisha kazi msemaji wa huyo wa TFF FROLIAN KAIJAGE mpaka hapo uchunguzi dhidi yake utakapokamilika juu ya sakata hilo.
Rais wa TFF RODGER TENGA amesema kwa kushirikiana na wizara ya Habari Utamadunia na Michezo wanaunda kamati ambayo itachunguza chanzo cha tatizo hilo huku KAIJAGE akiwa nje mpaka hapo uchunguzi utakapokamilika.
Lakini katika hatua nyingine RODGER TENGA amesema ndani ya mwezi mmoja TFF inatarajia kutangaza nafasi mbili ya katibu wa TFF na msemaji wa TFF ili kuziba nafasi hizo haraka iwezekanavyo. Source Janejohn5.blog
No comments:
Post a Comment