Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Sep 20, 2010
TPDF na makakati wa kuboresha huduma zake!!
Mwandishi Wetu, JESHI la Wananchi Tanzania (TPDF) limesema litaendelea kushirikiana na kampuni, watu binafsi na mashirika mbalimbali katika kuhakikisha linaboresha huduma za kijamii kwa wanajeshi na familia zao. Akizungumza Dar es Salaam mwishoni mwa wiki Mkuu wa Kitengo cha Maduka, Vinywaji na Mikopo jeshini Meja C.J Kapandamtava alisema hatua hiyo pamoja na kujenga mahusiano na jamii ya kitanzania lakini pia itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wanajeshi wake kupata huduma wanazozitaka kwa wakati kulingana na mahitaji. Meja Kapandamtava aliyasema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa kinywaji kipya cha bia ya Kopo ya Heineken 25cl ‘Heineken Balozi ‘ maalumu kwa matumizi ya Jeshi iliyofanyika katika ukumbi wa jeshi wa kambi ya Lugalo Dar es Salaam. Alisema huduma za kijamii zinazopatikana katika maeneo ya makambi ikiwemo vinywaji vya aina mbalimbali havilengi kupata faida na kwamba hatua hiyo ni maalumu kwa wanajeshi kutokana na majukumu ya kitaifa waliyonayo. “Kuzinduliwa kwa kinywaji hiki jeshini kutatufanya tuendelee kuboresha wigo wa upatikanaji wa huduma za kijamii na kama tunavyojua sisi huku kwetu tunatoa huduma zaidi kuliko kulenga faida ikiwa ni utaratibu maalumu kwa jeshi kutokana na majukumu yao kitaifa,’ alisema. Aliwaasa wanajeshi kuitumia huduma hiyo kama ilivyolengwa na kuhakikisha kuwa vinywaji hivyo havipelekwi kwenye maduka uraiani. Kwa upande wake Kanali Harry Andrew Msechu aliyekuwa mgeni rasmi alisema jeshi kama mhimili mmojawapo wa taifa linapaswa kuangaliwa na kupewa huduma zenye ubora wa kimataifa kama kilivyo kinywaji hicho kinachotumiwa na nchi nyingi duniani. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mabibo Benedicta Rugemalira alisema ingawa bia ya Heineken tayari ilikuwepo jeshini katika ujazo wa 33cl bado wameona kuna umuhimu wa kupanua wigo wa kupatikana kwa kinywjai hicho hususani kwa kuzingatia bei. Alisema Heineken 33cl ya chupa yenye shingo fupi kwa kipindi kirefu imekuwa ikitumika jeshini na kuuzwa kwa sh. 1,300/- na kwamba kinywaji hicho kipya cha kopo katika ujazo wa 25cl kimeingizwa jeshini na kitauza kwa sh. 1,000/-. Alisema hatua hiyo ni katika kuwajali wanajeshi kutokana na majukumu mazito waliyonayo katika ujenzi wa taifa na kwamba hiyo ni sehemu ya uwajibikaji wa kampuni hiyo kwa jamii ya kitanzania kulingana na majukumu yanayowakabili. Rugemalira aliongeza kwa kushukuru uongozi wa Makao Makuu ya Jeshi hususani upande wa vinywaji kutokana na ushirikiano mkubwa wanaoupata na kwamba kampuni hiyo itahakikisha mahusiano hayo yanaendelea kudumishwa kadri siku zinavyoendelea. “Tayari tulikuwa na Heineken jeshini lakini kwa ujazo wa 33cl inayouzwa sh. 1,300/- na kwamba bei hii wakati fulani ilikuwa inawanyima haki wale waliokuwa na uwezo mdogo hivyo tumeona tupeleke kinywaji kingine kwa bei ambayo wengi wataimudu,tunawashukuru jeshi kwa ushirikiano wanaotupa,” alisema Rugemalira.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment