


Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Miss Progress International Juliet Willy akipozi kwa picha mara alipowasili akitokea nchini Italia alikoshiriki shindano la urembo katika taji hilo na kufanikiwa kutwaa taji hilo la Dunia ambalo ndiyo kwanza limeanzishwa mwaka huu, hivyo kuwatoa kimasomaso watanzania katika nyanja ya Urembo. Juliet amekwa mrembo wa kwanza Tanzania kutwaa taji la dunia katika masuala ya urembo na warembo wengi wameshiriki katika mashindano tofauti tofauti ya dunia lakini bado hawajafanikiwa kufikia katika kutwaa taji la dunia.
Rosemary Momburi Mama mzazi wa Miss Progress International Juliet Willy akimkabidhi ua kama ishara ya kumkaribisha nyumbani Tanzania mara baada ya kufanya vyema na kutwaa taji la dunia linalojulikana kama Miss Progress International.
Miss Progress International Juliet Willy katikati akipungia mashabiki ndugu na jamaa waliokuja kumpokea kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jijini Dar es salaam mara baada ya kuwasili akitokea nchini Italia, kulia ni Caroline Sanga Mwandaaji wa Mashindano hayo Tanzania na kushoto ni Rosemary Momburi mama mzazi wa Juliet Willy. 


Mgombea urais kwa tiketi ya CCM Dr.Jakaya Kikwete akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Shinyanga jana jioni (Picha na Freddy Maro na Muhidin Michuzi)
Jakaya Kikwete mara baada ya kutua kwa helikopta nje ya uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga leo Jumatatu na kuamua kutembea kwa miguu hadi uwanjani
Mwanachama Mkongwe wa CCM Bi.Fatma Ndugulile akimuonesha Mwenyekiti wa CCM Dr.Jakaya Mrisho Kikwete kadi yake ya uanachama na risiti za malipo ya mwanachama tangu mwaka 1977 wakati Bibi huyo alipokutana na Mgombea huyo wa Urais kwa kupitia CCM mjini Shinyanga jana jioni. Dr.Kikwete alimsifu Bibi huyo kwa uaminifu wake kwa CCM na umahiri wake wa kutunza risiti zake za malipo. | Kinamama waliokuwa wakimsubiri kwa hamu JK katika uwanja wa Kambarage mjini shinyanga wakirukaruka kwa furaha mara helikopta ya JK ilipokuwa ikitua nje ya uwanja huo. |



Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga akitoa shukrani mara baada ya kukabidhiwa cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi
Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries Limited Bw. Ajay Mehta akishukuru mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries Limited Bw. Ajay Mehta.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga ambaye aliambatana na Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mtahaba.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinazotambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru katikati ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi. Mwamvita Makamba.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Msaidizi wa Kampuni ya Azam Bw. Yusuph Kamau katikati ni Meneja Biashara wa kampuni hiyo ya Azam Bw. Daniel Hill aliyembatana nae.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Kampuni ya Chemi&Cotex Industies LTD, Bw. Lakshmi Narayan, Katikati ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Chemi&Cotex Industries LTD, Bw. Riyan Dewji. (Picha kwa hisani ya www.michuzijr.blogspot.com).· Ni kwa Face Book na nyinginezo
Dar es Salaam, 26 Septemba, 2010. Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua huduma mpya ya Intaneti ambayo itawawezesha wateja wake kuchati kwa intaneti bure.
Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi Mwamvita Makamba alisema jana kwamba wateja wa Vodacom sasa wanaweza kuchati bure kwenye tovuti za Face Book, the Grid na Vodamail.
Alisema Vodacom Tanzania inatoa huduma hiyo kwa lengo la kuwawezesha wateja wake kupata muda wa kuchati zaidi.
Alifafanua kwamba hayo yote yatawezekana kwa kutumia mtandao wa 3G ambao una kasi na nguvu kubwa.
“Tunapenda wateja wetu watumie mtandao wetu kwa kuwasiliana bure na hivyo kukata kiu yao ya mawasiliano”.
Alitoa wito kwa wateja wa Vodacom na Watanzania kwa ujumla kutumia huduma hiyo ya mtandao wa Intaneti.
Aliwaomba Watanzania kujiunga na Vodacom ili kupata huduma hiyo bure na hivyo kuwasiliana zaidi.
Alisema huduma hiyo itapatikana kwa simu za mkononi na pia kwa Laptop zilizounganishwa na USB Moderm.
Tangu kuanzishwa kwake miaka kumi iliyopita Vodacom imekuwa ikizindua huduma mpya kila mara kwa lengo la kurahisha huduma za mawasiliano kwa wateja wake.
Hivi sasa kampuni hiyo inawateja zaidi ya milioni saba ambao wanaunganishwa na huduma mbalimbali zenye lengo la kuboresha maisha yao, baadhi ya huduma hizo ni kama M-Pesa, ambayo ni njia ya haraka na uhakika ya utumaji wa pesa hapa nchini.
Vodacom ndiyo wa kwanza kuanzisha huduma hiyo hapa nchini.
| Wanachama Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Lindi mjini wakimsikiliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati alipokuwa akiwahutubia.Picha na Mwanakombo Jumaa |

