
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 13, 2010
Rais Jakaya atambua mchango wa wakulima!!

ANDREW CHALE ASEMA VIJANA TUSIWE MITAJI YA WAGOMBEA!!
Vodacom Tanzania yamwaga Vifaa kwa Vilabu Ligi Kuu!!
Rais Kikwete afungua mkutano mkuu wa Tanganyika Law Society Dodoma!!
Aug 12, 2010
SHIRIKISHO LA MUZIKI NALO LAPATA VIONGOZI WAO!!!
Na Alistide Kwizela.
Hatimaye Shirikisho la Wanamuziki Tanzania leo (Jumatano) limepata viongozi wake wa muda katika uchaguzi uliofanyika kwenye Ukumbi wa BASATA na kusimamiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa COSOTA,Bw.Yunus Mkinga.
Katika uchaguzi huo uliokuwa wa vuta ni kuvuta,Bw.Ibra Washokera aliweza kuibuka kidedea kwenye nafasi ya urais baada ya kupata kura 12 na kumbwaga Mkongwe wa muziki wa dansi,Hamza Kalala ‘Komandoo’ aliyeambulia kura 2 tu.
Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais,Mwanamuziki wa muziki wa asili,Che Mundugwao aliibuka kidedea kwa kupata kura 9 na kuwaacha mbali wapinzani wake ambao ni Mkongwe Kassim Mapili na Gwalugano Ayoub walioambulia kura 3 kila mmoja.
Nafasi ya Katibu ilichukuliwa na Salum Mwinyi huku nafasi ya Mkurugenzi wa Fedha na Mipango ikikamatiwa na Samwel Semkuto.Aidha, wajumbe waliochaguliwa ni Samatha Rajab, Said Mukandara na George Mbata.
Wakiongea kwa kwa nyakati tofauti baada ya uchaguzi, Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego,Bw.Yustus Mkinga na Mlezi wa Mashirikisho ya wasanii,Mzee Rashid Masimbi walisema kwamba, kazi iliyopo mbele ni kwa viongozi hao kupanga mikakati ya muda mfupi na muda mrefu ya kuwaendeleza wasanii na kupigania maslahi yao.
Aidha, walisisitiza kwamba, kwa sasa wasanii wa muziki wanatakiwa kusimama imara chini ya shirikisho lao na kuwa na msimamo thabiti katika masuala mbalimbali yanayowahusu.
Kesho itakuwa ni zamu ya uchaguzi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi na keshokutwa ni shirikisho la Sanaa Jongevu (Filamu),Wadau wote mnakaribishwa kwenye chaguzi hizo ambazo ni maendeleo makubwa kwa wasanii na sekta ya sanaa kwa ujumla.
Miss Universe 2010 kwisha kwiva mjini Vegas!
RAMADHAN KAREEM

May Allah grant you the strength and yaqeen to complete this blessed month of Ramadhan
And may you take full advantage of these powerful days, Insha-Allah.
May I take this opportunity to wish you, your family, friends and loved
ones, A Blessed Month of Ramadhan...
May Allah's mercy and blessings be with you throughout the Holy month of
sacrifice and throughout the year, Insha-Allah.
May all your good deeds & du'as be accepted, your wishes fulfilled and all your sins forgiven.
May Allah grant us the strength to help those less fortunate in Allah's
name, Insha-Allah!
Have a splendid Ramadhan!
Remember me & my family in your Du'as
*WANACHAMA WA CCM DAR WAANDAMANA KUMPINGA MGOMBEA ALIYEPITISHWA NA KUACHWA WALIYEMCHAGUA
WAZIRI WA KAZI PROF.KAPUYA AZINDUA MWAKA WA VIJANA!!
Mikoko ya Vodacom kukuza uchumi kwa washindi!!
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yakabidhi vifaa Tiba Dodoma!!
BLOOD DIAMONDS - A TRAGEDY OF HISTORIC PROPORTION!!

MWENYEKITI WA (YUNA) HAPA NCHINI AWAPA CHANGAMOTO VIJANA!!
Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa nchini YUNA Bw. Benny Kikove wakati alipokuwa akiongea na wajumbe wa konamano hilo asubuhi hii.
TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS NGUVU SAWA!!
Precision Air yaleta ndege mpya!!

WAGOMBEA UBUNGE WA CUF (W) ILALA WAJITAMBULISHA!!
MAOFISA HABARI WAKUTANA LEO JIJINI DAR.
Aug 11, 2010
BASATA KUYAPA MENO RASMI MASHIRIKISHO YA SANAA
Mchakato huo utakaodumu kwa siku nne hadi Ijumaa umeanza kwa Shirikisho la Wasanii wa Sanaa za Ufundi kuchagua viongozi wao wa muda ambao watasimamia kikamilifu utayarishaji wa kanuni za kuliongoza shirikisho hilo na baadaye kuitisha uchaguzi utakaowaweka viongozi wa kikatiba.
Katika uchaguzi huo uliosimamiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni Kutoka Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Bi.Angela Ngowi, Bw.Adrian Nyangamale ambaye ni Rais wa Chama cha Wasanii wachoraji alichaguliwa kuwa Rais wa Muda wa Shirikisho hilo baada ya kupata kura 12 kati ya 21 zilizopigwa na kuwabwaga wenzake ambao ni Gwalugano Lyimo na Focus Senya.
Kwa upande wa Makamu wa Rais,Mwanamitindo maarufu nchini,Khadija Mwanamboka aliibuka kidedea baada ya kupata ushindi wa kishindo wa kura 18 kati ya 21.Nafasi ya Katibu ilikwenda kwa Godfrey Ndimbo huku mweka hazina akichaguliwa Rashidi Mbogo.
Wajumbe walioteuliwa kuliongoza jahazi la shirikisho hili ni pamoja na Rashidi Munyana,Basil Nyambele na Gwalugano Ayoub.
Akizungumza baada ya Uchaguzi,Msimamizi wa uchaguzi Bi.Ngowi alisema kwamba,huo ni mwanzo wa wasanii kujisimamia na kujipanga kwa ajili ya kutetea maslahi yao na kuhakikisha wanalinda haki ya kazi zao na kutafuta masoko kwa ajili ya kazi zao.
Aliongeza kwamba,viongozi waliochaguliwa lazima wahakikishe wanasimamia kikamilifu katiba na kutafuta fursa na mbinu za kupenya kwenye soko la pamoja la Afrika Mashariki.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alisema kwamba, lengo la Baraza ni kuona wasanii wanakuwa na umoja wa kitaifa na Kutoka kwenye makucha ya utegemezi na kupambana mmojammoja.Aliongeza kwamba, wakati umefika kwa wasanii kuonesha usasa na kuachana na ufanyaji kazi za sanaa wakiwa katika mazingira yasiyo rasmi na ya kulalamika tu bila kuwa watendaji na watekelezaji.
Mlezi wa Wasanii wa Sanaa za Ufundi,Rashid Masimbi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya BASATA alisema kwamba, kazi iiyopo mbele ni kwa viongozi waliochaguliwa kuja na mipango ya muda mfupi na mrefu katika kulikuza shirikisho, kutafuta wanachama wapya na kuandaa kanuni za kuliendesha shirikisho hilo.
BASATA liko kwenye mkakati kabambe wa kujenga umoja wa wasanii kupitia mashirikisho ambapo sasa wasanii nchi nzima watakuwa na fursa ya kuwa na sauti moja pia kupanga misimamo yao itakayoheshimika kitaifa na kimataifa.
Mashirikisho ambayo yameundwa na sasa uongozi wake unatafutwa ni yale ya Sanaa za Ufundi,Sanaa za Muziki,Sanaa Jongevu (Filamu) na Sanaa za Maonesho.
Baraza linawataka wasanii wote, kuhakikisha wamejisajili na kujiunga na mashirikisho hayo kwa ajili ya kuanza mkakati wa kutetea maslahi yao.
RATIBA KAMILI YA CHAGUZI KATIKA MASHIRIKISHO
1. Jumatano,Agosti 11, 2010-Shirikisho la Muziki Tanzania,Kwenye Ukumbi wa BASATA kuanzia saa 4.00.Asubuhi.
2. Alhamisi,Agosti 12,2010-Shirikisho la Sanaa za Maonesho,Ukumbi wa BASATA kuanzia Saa 4.00 Kamili.
3. Ijumaa Agosti 13, 2010-Ahirikisho la Sanaa za Jongevu (Filamu) Tanzania, Ukumbi wa BASATA kuanzia saa 4.00.
Matokeo yatatangazwa kwnye vyombo vya habari,
WADAU WOTE MNAKARIBISHWA,
Habari na Alistide Kwizela,Afisa Habari wa BASATA.
Ukweli Kuhusu Haruna Moshi ‘ Boban’ : Alikosa Namba Gavle IF
