| Hapa katika picha anaonekana akimnadi Mgombea ubunge jimbo la Nkenge Bukoba Vijijini mama Assumpta Mshana |
| Kikundi cha watoto wa shule ya awali ya Kitobo Misenyi Bukoba vijijini wakimkaribisha Mke wa Rais Mama SALMA Kikwete |
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
| Hapa katika picha anaonekana akimnadi Mgombea ubunge jimbo la Nkenge Bukoba Vijijini mama Assumpta Mshana |
| Kikundi cha watoto wa shule ya awali ya Kitobo Misenyi Bukoba vijijini wakimkaribisha Mke wa Rais Mama SALMA Kikwete |
Mgreni rasmi katika harambee ya kuchangia Juhudi za CCBRT katikakusaidia watoto wenye matatizo Bw. Januari Makamba akizungumza mbele ya wageni waalikwa katika harambee hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Double Tree maeneo ya Masaki jijini Dar es salaam ambayo inaendelea usiku huu. Januari Makamba amewataka watanzania kusaidia watoto wenye matatizo ili nao waweze kupata mahitaji muhimu kama watoto wengine na kuwapunguzia matatizo watoto hao.
Mkurugenzi wa Shear Illution Shekha Nasser akisoma hotuba yake mbele ya wageni waalikwa mbalimbali katika harambee ya kuchangia juhudi za CCBRT katika kusaidia watoto wenye matatizo.
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima Absalom Kibanda akipata picha na Mbunge mtarajiwa wa jimbo la Bumbuli mkoani Tanga Januari Makamba.
Mboni Masimba kushoto, Fiderin Iranga katikatio pamoja na rafiki yao nao walipenda kuchangia harambee hiyo.
Mgeni rasmi January Makiamba akiwa katika mpicha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shear Illution Shekha Nasser ambaye ndiye aliyeandaa harambee hiyo.
Mbunge Mtarajiwa wa Jimbo la Bumbuli Januari Makamba wa pili kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba kulia kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa na katikati ni Lissa Jensen aliyewahi kuwa Miss Tanzania.
Mkurugenzi wa Shear Illutions, Shekha Nasser akisoma hotuba yake mbele ya wageni waalikwa mbalimbali katika harambee ya kuchangia juhudi za CCBRT katika kusaidia watoto wenye matatizo.
Mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia Juhudi za CCBRT katika kusaidia watoto wenye matatizo,Bw. Januari Makamba akizungumza mbele ya wageni waalikwa katika harambee hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar usiku huu.Bw. Januari Makamba amewataka watanzania kusaidia watoto wenye matatizo ili nao waweze kupata mahitaji muhimu kama watoto wengine na kuwapunguzia matatizo waliyonayo.
Baadhi warembo wakiwa katika picha ya pamoja pindi waliposhiriki katika tukio la Shear Charity Ball usiku huu,ndani ya hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar. 
Ma Mc wa shughuli hii maalumu iliofanyika usiku huu ndani ya moja ya ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Double Tree Hilton,shoto ni Taji Liundi pamoja na Penny.

Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akiwahutubia mamia ya wanawake, wanachama wa UWT na wanachi waliohudhuria Sherehe za Maadhimisho ya Wiki ya Wanawake Tanzania Kitaifa zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es salaam leo Okt 2. (Picha zote na Muhidin Sufiani)
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipokea Kadi ya Leila Seif, aliyekuwa Mjumbe wa Baraza la Wanawake wa Chama cha CUF, aliyejiunga na CCM na kukabidhi kadi ya CUF wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Wiki ya Wanawake Tanzania iliyofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma leo Okt 2.
Wasanii wanaounda kundi la Lady Eyes kutoka (kushoto) Luiza Mbutu, Vicky Kamata, Mwacity Almas, Nyota Waziri na Stara Thoma, wakiimba kwa pamoja kibao maalum kutoa burudani wakati wa Maadhimisho ya Sherehe hizo zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Wanamuziki wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ wakishambulia jukwaa kutua burudani wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Wanawake Tanzania UWT Kitaifa iliyofanyika leo Okt 2 kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Mama Maria Nyerere na Mama City Mwinyi, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma leo Okt 2 kuhudhulia Sherehe za Maadhimisho ya Wiki ya Wanawake Tanzania Kitaifa, iliyofanyika leo kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Mwananyamala Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam.
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na wanachama wa CCM na Wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Mwananyamala A jijini Dar es Salaam, katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wiki ya Wanawake Tanzania Kitaifa leo.
Mgombea Mwenz a wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal na mkewe Bi Zakia Bilal, wakiingia kwenye Uwanja wa CCM Mwinjuma Mwananyamala Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo Okt 2, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wiki ya Wanawake Tanzania (UWT) na Mkutano wa kampeni .
Mwanamitindo Machachari Fiderin Iranga akipita na vazi la Khanga jukwaani katika onesho la Usiku wa Khanga onesho lililoandaliwa na mbunifu wa mavazi Asia Idarous kutoka kampuni ya Faback Fashion, onesho hilo linafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee VIP usiku huu jijini Dar es salaam. Hivi sasa nahamia upande wa pili katika ukumbi huu huu wa Diambond Jubilee ambako kuna onesha la kukata na shoka la mwanamuziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Ferre Golla (Shetani) ambaye anafanya onesho pamoja na bendi ya Mashujaa ya jijini Dar es salaam usiku huu.
Mbunifu wa mavazi kutoka kampuni ya Kapwani Grace Sinamtwa akiwa katika picha ya pamoja na Mathew aliyevaa shati lililobuniwa na mbunifu huyo.