Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Sep 28, 2010
Dk Siame akaidi kuvunja kambi za wana CCM Mbozi
Oiko Credit yakopesha Bil 2.1/- kwa YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo ili kuiwezesha jamii
Meneja wa mradi wa ukarabati wa jengo la YWCA Moshi, Elimringi Maringo akimuongoza Meneja wa Oiko Credit Tanzania, Deus Manyenye kuangalia hali ya ujenzi inavyoendelea mara baada ya kukabidhi hundi yenye thamani ya milioni 500/- kwa YWCA Moshi, fedha ambazo zimetolewa kwa mkopo kwa ajili ya ukarabati wa jengo la chama hicho lililokaa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo. Waliongozana nae ni makamu mwenyekiti wa chama hicho Vicky Lyimo.
Meneja wa Oiko Credit Tanzania Deus Manyenye akizungumza na Mwenyekiti wa Saccos ya Wazalendo, Mbonea Maghimbi (kulia), makamu mwenyekiti wa chama hicho Vicky Lyimo (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa YWCA Moshi, Valentine Mwinga kuhusiana na aina ya mikopo wanayotoa mara baada ya hafla kukabidhi hundi zenye thamani ya bilioni 2.1/- kwa YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo zote za mjini humo.
Na Mwandishi Wetu, Moshi
KAMPUNI ya OIKO Credit inayojishughulisha na ukopeshaji fedha kwa taasisi mbalimbali duniani zikiwemo benki, imezikopesha jumla ya shilingi bilioni 2.1/- YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo ili zitumike kuiwezesha jamii ya watu wa kipato cha chini.
Fedha hizo zinazotumika kwa ajili ya ukarabati wa jengo la makao makuu ya YWCA Moshi na uwezeshaji jamii ili ijiendeleze kimaisha kupitia Wazalendo ni muendelezo wa mikopo kutoka kampuni hiyo iliyoitoa katika kipindi cha mwaka huu kwa taasisi 12 nchini unaofikia jumla ya bilioni 8.2/-
Akizungumza jana mjini hapa wakati wa hafla ya kukabidhi hundi Meneja wa Oiko Credit Tanzania Deus Manyeye alisema kuwa lengo la kampuni yake ni kuwekeza kwenye taasisi za fedha zilizolenga kuiendeleza jamii ya kipato cha chini duniani.
Akifafanua Manyeye alibainisha kwamba licha ya kupokea maombi mengi lakini wamehakikisha fedha wanazotoa zinaelekezwa kwenda kusaidia miradi ya uzalishaji inayolenga watu wa hali duni wanaopigania kujikwamua kutoka kwenye umaskini.
“Tulichunguza na kubaini kwamba YWCA Moshi na Wazalendo Saccos wamekidhi vigezo vya kupewa mikopo kwani walikuwa na nia ya dhati ya kuikomboa jamii ya chini kutoka kwenye umaskini unaoikabili. Tayari fedha zimeshaanza kutumika kama mnavyoona ukarabati wa jengo hili unavyoendelea,” alisema Manyeye.
Aidha kwa kuwa idadi ya watu Tanzania ni kubwa kuliko ile ya Kenya na Uganda taasisi hiyo imepanga kuziwezesha kwa kuzikopesha zaidi asasi na wadau wa nchini ili waweze kuhudumia kundi kubwa la watu kuliko ilivyo sasa ambapo nchi hizo zimekuwa zikipata fungu kubwa la fedha.
Kwa upande wake Katibu wa YWCA, Frida Mbowe alisema kwamba kwa kuwa manispaa hiyo inajiandaa kuwa hadhi ya jiji mkopo huo wa milioni 500/- utawawezesha kukarabati jengo kuwa lenye muundo wa kisasa utakaotoa mvuto kwa wawekezaji kupangisha na kufungua ofisi mbalimbali.
Naye Mbonea Maghimbi ambaye ni mwenyekiti wa Wazalendo aliishukuru Oiko Credit kuwakopesha bilioni 1.6/- na kusema watazitumia kama ilivyokusudiwa kwa kuwawezesha watu wa kipato cha chini kuweza kuinua hali yao kimaisha.
“Mbali na hilo pia tumepanga kuzitumia fedha hizo kutoa elimu kwa jamii inayotuzunguka umuhimu wa kujenga utamaduni wa kuhifadhi ama kujiunga na Saccos ya Wazalendo na faida mbalimbali watakazonufaika nazo mara watakapotimiza vigezo,” alisema Maghimbi.
Tangu Oiko Credit yenye makao makuu yake nchini Uholanzi ilipoanzishwa nchini mwaka 2006 imejiongezea wateja kutoka sekta mbalimbali ikiwemo benki, SME’s, Saccos, Makanisa na kuwekeza kutoka milioni 260/- hadi kufikia bilioni 16 Juni mwaka huu kutoka wateja wawili hadi 21
dr. bilal aendelea na ziara za kampeni mkoani iringa
HOSPITALI YA REGENCY KUJENGA KITUO KIPYA CHA AFYA
taasisi ya superbrands yaingia Tanzania
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga akitoa shukrani mara baada ya kukabidhiwa cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi
Sep 27, 2010
mbio za mashua bahari ya hindi zawa kivutio
ridhiwani kikwete ndani ya chunya mkoani mbeya
Sep 26, 2010
Wateja wa Vodacom sasa kuchati bure kwa Intaneti
· Ni kwa Face Book na nyinginezo
Dar es Salaam, 26 Septemba, 2010. Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua huduma mpya ya Intaneti ambayo itawawezesha wateja wake kuchati kwa intaneti bure.
Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi Mwamvita Makamba alisema jana kwamba wateja wa Vodacom sasa wanaweza kuchati bure kwenye tovuti za Face Book, the Grid na Vodamail.
Alisema Vodacom Tanzania inatoa huduma hiyo kwa lengo la kuwawezesha wateja wake kupata muda wa kuchati zaidi.
Alifafanua kwamba hayo yote yatawezekana kwa kutumia mtandao wa 3G ambao una kasi na nguvu kubwa.
“Tunapenda wateja wetu watumie mtandao wetu kwa kuwasiliana bure na hivyo kukata kiu yao ya mawasiliano”.
Alitoa wito kwa wateja wa Vodacom na Watanzania kwa ujumla kutumia huduma hiyo ya mtandao wa Intaneti.
Aliwaomba Watanzania kujiunga na Vodacom ili kupata huduma hiyo bure na hivyo kuwasiliana zaidi.
Alisema huduma hiyo itapatikana kwa simu za mkononi na pia kwa Laptop zilizounganishwa na USB Moderm.
Tangu kuanzishwa kwake miaka kumi iliyopita Vodacom imekuwa ikizindua huduma mpya kila mara kwa lengo la kurahisha huduma za mawasiliano kwa wateja wake.
Hivi sasa kampuni hiyo inawateja zaidi ya milioni saba ambao wanaunganishwa na huduma mbalimbali zenye lengo la kuboresha maisha yao, baadhi ya huduma hizo ni kama M-Pesa, ambayo ni njia ya haraka na uhakika ya utumaji wa pesa hapa nchini.
Vodacom ndiyo wa kwanza kuanzisha huduma hiyo hapa nchini.
ziara ya mama salma kikwete mkoani lindi
Wanachama Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Lindi mjini wakimsikiliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati alipokuwa akiwahutubia.Picha na Mwanakombo Jumaa |
dr. bilal mkoani kagera
Sep 25, 2010
Jk Aifunika musoma uwanja wa Mkendo!!
Maalim Seif aahidi kupunguza kodi zanzibar
DK. BILAL AVUNA KADI LUKUKI ZA WAPINZANI BUKOBA
wanja la dr. kikwete na dr. bilal
Sep 24, 2010
P - FUNCK ATOA UFAFANUZI
SERIKALI KUDHIBITI WAGANGA NA WAKUNGA WA TIBA ASILIA WANAKIUKA SHERIA!!
MAGRETH KINABO NA ARON MSIGWA- MAELEZO
SERIKALI imeagiza kuwa kila halimashuri ya wilaya,miji, manispaa na majiji iwe na Mratibu wa Tiba Asili ambaye atakuwa msimamizi wa masuala ya hayo, ikiwa ni hatua ya kuwadhibiti watoa huduma wa tiba hiyo watakaokiuka sheria.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni kwa niaba yake wakati uzinduzi wa usajili wa waganga wa tiba asili nchini.
“Mratibu huyu awe ni mfanyakazi katika idara ya afya aliyechini ya Mganga Mkuu wa Halimashauri husika,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Waziri Mkuu alisema hayo huku akiagiza kuwa waganga wanaofanya matendo yanayohatarisha uhai wa watu yanayohusisha waganga wa tiba asili ambayoni uuaji wa vikongwe, albino, watoto wadogo na uchunaji wa ngozi za binadamu kuwa hawatakuwa sehemu ya wizara hiyo.
“Yeyote atakayebanika kujihusisha na vitendo hivyo, wizara haitamtambua kuwa ni mganga na hivyo hatasajiliwa na kuruhusiwa kutoa huduma ya asili,” alisisitiza huku akisema waganga na wakunga na hasa waganga wa tiba asili nchini wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo yakiwemo maelekezo mbalimbali ya wizara hiyo.
Aliongeza kuwa waganga hao wanatakiwa kuanzisha vituo rasmi, kutoa huduma kwa mfumo wa kitaasisi na si mtu mmojammoja , kutayarisha dawa katika mazingira safi kujiendeleza kielimu na kuanzisha vitalu na mashamba ya miti dawa ili kuhifadhi dawa na mazingira ikiwemo kutunza kumbukumbu.
Akizungumzia kuhusu usajili huo, Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Deo Mutasiwa alisema waganga na wakunga wa tiba asili wataruhusiwa kusajiliwa kwa mujibu wa sheria namba 23 ya mwaka 2002 na kanuni zake. Hivyo watakaokiuka wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria.
Dk. Mutasiwa aliongeza suala la usalama wa dawa za tiba hizo litasimamiwa na Serikali chini , Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA), lakini la kuhusu jukumu la dawa na jinsi inavyofanya kazi litakuwa na mwenyewe dawa .
Na Mwakilishi Shirika la Afya Duniani Tanzania (WHO) Dk. Rufaro Chatora, alishauri wanasayansi kufanya utafiti wa dawa za asilia ili kuboresha huduma hiyo. Pia utafiti wa dawa hizo ukishirikisha na ule dawa za kisasa ufanyanyike ili kuimarisha na kuendeleza huduma hizo kwa kisasa.
AFANDE ACHEZEA KICHAPO TOKA KWA MAJANI
P.Funk kapigiwa simu now ikiwa ONLINE East Africa Radio na kusema kuwa amelala wampigie baadae, na nia yakumpigia ni kwamba walitaka kujua upande wa pili wa P.Funk.
(Kwa niaba ya NAY WA MITEGO aliyeshuhudia chezo pale bongo recordz)
NITATEKELEZA ILANI YA CCM KWA KASI ZAIDI, NGUVU ZAIDI NA KUWAPA VIJANA AJIRA,MO DEWJI…!!!
MO akihutubia wananchi wa Kata ya Unyambwa.
*******************
Na Hillary Shoo.
Singida. Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM, Mohamed Gulam Dewji, amesema endapo wananchi watampa ridhaa ya kuendelea kuwawakilisha tena bungeni, atatekeleza Ilani ya CCM kwa kasi zaidi ikiwemo kutafuta ufumbuzi wa namna ya kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana.
Dewji alisema katika ilani uchaguzi, CCM imeainisha wazi kwamba inatambua tatizo la ajira na hasa ajira ya vijana wanaomaliza elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu kila mwaka kuwa, ni kubwa mno.
“Vijana hawa wote ni nguvu kazi ya taifa ambayo inaweza kutumika katika kazi na shughuli halali za ujenzi wa nchi yetu na ikapiga hatua kubwa ya kimaendeleo”,alisema Dewji.
Mgombea huyo,alisema ili kukabiliana na tatizo hilo, CCM ina mpango wa kupanua mafunzo ya VETA yaweze kuchukua vijana wengi zaidi, ili waandaliwe kujiajiri wenyewe.
Aidha, alisema vijana watahamasishwa kuanzisha miradi ya kiuchumi na kujiunga katika vikundi vya ushirika vya kuweka na kukopa (SACCOS) ili waweze kupata mikopo kwa masharti nafuu.
“Katika miaka mitano iliyopita, nimewatafutia kazi vijana kutoka jimboni kwetu kwenye kiwanda changu cha nguo cha Afritex kilichopo mkoani Tanga., Kuajiri vijana hao, nimefanikiwa kwa kiasi fulani kupunguza idadi ya vijana wetu wanaomaliza elimu ya sekondari, kukaa vijiweni”,alisisitiza huku akishangiliwa na mamia ya wananchi.
Dewji aliyasema hayo jana katika mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Unyambwa.
Wakati huo huo,Dewji alitumia fursa hiyo kumwombea kura mgombea urais Jakaya Kikwete kwa madai kwamba ameonyesha uwezo mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa ilani za uchaguzi. Aidha, alimnadi mgombea wa udiwani wa kata hiyo, ya Unyambwa Salum Satu na kuomba apewe kura za kutosha kumwezesha kushika nafasi hiyo.
MO, akisistiza kuwa Katika kipindi cha miaka saba michezo imeweza kupaa katika mkoa wa Singida ambapio Kindai Shooting Stars, timu ya mkoa ilibeba kombe la kilimanjaro Taifa Cup kwa mara ya kwanza katika historia ya mkoa huo.
MO akizcheza ngoma ya Kinyaturu ya kutikisa mabega, maarufu kwa jina la tikisa mabega tingisha kiuno.
Wanafunzi wa shule ya msingi Unyambwa wakimpokea MO kwenye viwanja vya shule hiyo wakati alipokwenda kweye mkutano wa kampeni wa Kata hiyo.
Wanafunzi wakiwa na mabango yanayomnadi MO huko KatikaKata ya Unyambwa.
Visura 10 kuonesha mavazi yaliyooneshwa na Mustafa Hassanali nchini Cameroon February na Zanzibar Julai 2010.
Mwanzilishi na muandaaji wa jukwaa la wanawake wajasiriamali Tanzania (TWENDE ) na Jukwaa la kukuza vipaji vya wabunifu chipukizi Swahili Fashion Week, ambae pia ni mbunifu maarufu wa mavazi, Mustafa Hassanali amealikwa kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya mavazi yanayofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku mbili tarehe 23 na 24 ya mwezi huu katika hoteli ya New Arusha.
Maonyesho hayo yameandaliwa na Maridadi. Maridadi ni kikundi kinachojumisha wanawake watatu kutoka mataifa tofauti ya Tanzania, Austarialia na Uholanzi ambao wanaishi nchini katika jiji la Aruha na kujishughulisha na masuala mbalimbali yanayohusiana na mendeleo ya mwanamke..
Akielezea lengo la kuandaa maonyesho hayo, mmoja wa wanawake hao, Lilian Bulengo
amesema kuwa “dhumuni kuu la kuandaa tukio hili linalojulikana kwa jina la “Maridadi Women Show” ni kuwakutanisha pamoja wanawake kutoka maeneo tofauti ya Arusha na Moshi katika Fashion Show, maonyesho ya biashara pamoja na kupata fursa ya kuzungumza mambo mbalimbali yanayowakabili wanawake katika maisha ya kila siku hapaTanzania ikiwemo suala la unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji, wanawake na kuondokana na utegemezi na masuala ya uchumi na biashara kwa ujumla”.
Mustafa Hassanali, pamoja na kuwa mgeni rasmi, pia ataonyesha mavazi ambayo kwa mara ya kwanza alionyesha nchini Cameroon mezi wa 2 mwaka huu katika show iliyojulikana kama PARFUM D’AMOUR, na mavazi yanayojulikana kwa jina la Karafuu collection aliyoyaonyesha julai 2010 Zanzibar.
Jumla ya visura 10, kati yao nane kutoka Dar es salaam na wawili kutoka Arusha watapita jukwaani na kuonyesha mavazi hayo ya Mustafa Hassanali, ambayo yanawavutia wengi kutoka na ubunifu wa hali ya juu.
“Nimefurahi sana kupata fursa ya kuwa mgeni rasmi katika tukio hili, pia kuonyesha nguo zangu ambazo zilipendwa sana Cameroon, naamini pia wakaazi wa Arusha watafurahia kazi yangu” . Alisema Hassanali.
Katika maonyesho haya Mustafa ataonyesha na wabunifu wengine kutoka Arusha ambao ni Shwari Collectables,Hanifa Hash na Woolworth.
Mbali na maonyesha hayo pia siku ya jumamosi kutakuwa na manyesho ya kibiashara yatakayojumuisha kazi mbalimbali za sanaa za mikono. Benki nazo zitapata fursa ya kuonyesha na kuelezea shughuli zao mbalimbali wanazozifanya hasa katika kuchangia maendeleo ya wanawake Tanzania.