Sep 28, 2010

Dk Siame akaidi kuvunja kambi za wana CCM Mbozi

Na Richard Mwaikenda, Mbozi.
MGOMBEA ubunge Jimbo la Mbozi Magharibi, Dk. Lukas Siame,ametakiwa kuvunja makambi na kuwaomba radhi wananchi aliowakosea wakati wa mchakato wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili kujenga umoja na mshikamano utakaokifanya chama kishinde kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 31,mwaka huu.
Alishinikizwa kufanya hivyo na uongozi wa CCM Wilaya ya Mbozi na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano wa ndani wa kuweka mikakati ya kukipatia chama hicho ushindi wa kishindo uliofanyika juzi mjini hapa.
Ililazimika kumwambia hivyo, baada ya kubaini kuendelea kuwepo kwa makundi katika baadhi ya Tarafa jimboni humo,hali ambayo inaweza kuhatarisha chama hicho kukosa baadhi kura muhimu zinazohitajika kukipatia chama hicho ushindi wa kimbunga.
Jambo linginne lilowashitua ni kitendo cha mgombea huyo, kutamka wazi katika mkutano huo, kuwa yupo tayari kukosa kura za watu wasiokubali kuvunja makundi na kuungana naye katika kampeni na kwamba ana uhakikia kupata kura kwa watu wengine wanaomkubali.
"Naamini makundi yaliyojitokeza wakati wa kura za maoni tulizimaliza, na endapo kama kuna kundi halikubali kuvunja makundi , basi mimi niko tayari kuzikosa kura zao,lakini tutazipata kwa wengine wanaoniunga mkono,"alisema Dk. Siame..
Akihutubia katika mkutano huo, uliohudhuriwa pia na Mgombea ubunge jimbo la Mbozi Mashariki kupitia chama hicho, Godfrey Zambi, Mgeni rasmi, Ridhiwani alielezea kuwa si dhambi wakati wa kipindi cha mchakato wa uchaguzi wa kura za maoni kuibuka makundi, na kudai kwamba hiyo ni demokrasia ndani ya CCM, lakini makundi hayo yanatakiwa kuvunjwa mara moja anapotangazwa mshindi.
"Si dhambi wakati wa kipindi cha uchaguzi, kuwepo mgawanyiko maana hiyo ndio demokrasia ndani ya CCM,kwani si lazima unayempenda wewe basi kila mtu ampende,lakini utake usitake mwana CCM atakayeshinda katika mchakato huo na ambaye uongozi wa juu utamjadili na kurudisha jina lake,basi huyo ni wetu wote inatakiwa tumpiganie ashinde," alisema Ridhiwani.
"Kipindi cha kura ya maoni kilishapita, kinachotakiwa sasa ni wanaCCM kuwa na umoja pamoja na mshikamano utakaotuwezesha kukipatia chama chetu ushindi wa kishindo usioelezeka,"alisema Ridhiwani huku akishangiliwa. .
Ridhiwani, alikemea kitendo cha wapambe kuendelea kuwadhihaki wenzao waliokuwa kwenye kambi iliyoshindwa, na kuwataka waache mara moja tabia hiyo kwani haimsaidii mgombea,mwananchi na hata chama chenyewe.
"Wagombea na wapambe acheni kuwadhihaki na kuwakejeli wenzenu walioshindwa, tabia hiyo siyo nzuri, inawafanya wakichukie chama, tusahau yaliyotokea, tujirekebishe tulipokosea, tujenge umoja kwani kidole kimoja hakivunji chawa,"aliwaasa Ridhiwani.
Naye Mgombea ubunge Jimbo la Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi, alitamba kuwa kwa jinsi anavyoendesha kampeni zake ni dhahiri CCM jimboni humo itapata ushindi si chini ya asilimia 90,kwa vile katika kampeni amewashirikisha watu bila kujali anatoka kundi gani na kwamba hana kundi bali alilobakia nalo ni kundi moja tu la CCM.
Pia, Mwenyekiti wa UVCCM, Wilaya ya Mbozi,Jobu Kabinja, alisisitiza kauli zilizotolewa na baadhi ya viongozi kwa kumtaka Dk. Siame asiendelee na tabia ya kuzikataa kura za watu wasiotaka kuvunja makundi, kwa vile kura hizo wanazihitaji.
Naye Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo,Aloyce Mdaravuma, aliungana na viongozi wenzie, kwa kusema kuwa, wataungana na Dk. Siame kwenye kampeni kwa kuziomba kura kwa unyenyekevu hata kwa kulala chini mpaka kieleweke.
"Tutaingia kiume kwenye kampeni kwa kuzisaka kura katika Kata,vitongoji na nyumba kwa nyumba, hatutaki hata kura moja ipotee, kwani kura siyo zako ni za CCM,"alimazia kusema Mdaravuma.

Oiko Credit yakopesha Bil 2.1/- kwa YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo ili kuiwezesha jamii


Meneja wa Oiko Credit Tanzania Deus Manyenye (Kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya bilioni 1.6/- Mwenyekiti wa Saccos ya Wazalendo, Mbonea Maghimbi (kulia) fedha ambazo ni mkopo ili kusaidia kuwawezesha watu wa hali ya chini, Wakati wa hafla hiyo Oiko pia ilikabidhi hundi hundi yenye thamani ya milioni 500/- kwa YWCA Moshi kwa ajili ya ukarabati wa jengo la chama hicho lililokaa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo.
Meneja wa mradi wa ukarabati wa jengo la YWCA Moshi, Elimringi Maringo akimuongoza Meneja wa Oiko Credit Tanzania, Deus Manyenye kuangalia hali ya ujenzi inavyoendelea mara baada ya kukabidhi hundi yenye thamani ya milioni 500/- kwa YWCA Moshi, fedha ambazo zimetolewa kwa mkopo kwa ajili ya ukarabati wa jengo la chama hicho lililokaa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo. Waliongozana nae ni makamu mwenyekiti wa chama hicho Vicky Lyimo.
Meneja wa Oiko Credit Tanzania Deus Manyenye akizungumza na Mwenyekiti wa Saccos ya Wazalendo, Mbonea Maghimbi (kulia), makamu mwenyekiti wa chama hicho Vicky Lyimo (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa YWCA Moshi, Valentine Mwinga kuhusiana na aina ya mikopo wanayotoa mara baada ya hafla kukabidhi hundi zenye thamani ya bilioni 2.1/- kwa YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo zote za mjini humo.


Na Mwandishi Wetu, Moshi

KAMPUNI ya OIKO Credit inayojishughulisha na ukopeshaji fedha kwa taasisi mbalimbali duniani zikiwemo benki, imezikopesha jumla ya shilingi bilioni 2.1/- YWCA Moshi na Saccos ya Wazalendo ili zitumike kuiwezesha jamii ya watu wa kipato cha chini.

Fedha hizo zinazotumika kwa ajili ya ukarabati wa jengo la makao makuu ya YWCA Moshi na uwezeshaji jamii ili ijiendeleze kimaisha kupitia Wazalendo ni muendelezo wa mikopo kutoka kampuni hiyo iliyoitoa katika kipindi cha mwaka huu kwa taasisi 12 nchini unaofikia jumla ya bilioni 8.2/-

Akizungumza jana mjini hapa wakati wa hafla ya kukabidhi hundi Meneja wa Oiko Credit Tanzania Deus Manyeye alisema kuwa lengo la kampuni yake ni kuwekeza kwenye taasisi za fedha zilizolenga kuiendeleza jamii ya kipato cha chini duniani.

Akifafanua Manyeye alibainisha kwamba licha ya kupokea maombi mengi lakini wamehakikisha fedha wanazotoa zinaelekezwa kwenda kusaidia miradi ya uzalishaji inayolenga watu wa hali duni wanaopigania kujikwamua kutoka kwenye umaskini.

“Tulichunguza na kubaini kwamba YWCA Moshi na Wazalendo Saccos wamekidhi vigezo vya kupewa mikopo kwani walikuwa na nia ya dhati ya kuikomboa jamii ya chini kutoka kwenye umaskini unaoikabili. Tayari fedha zimeshaanza kutumika kama mnavyoona ukarabati wa jengo hili unavyoendelea,” alisema Manyeye.

Aidha kwa kuwa idadi ya watu Tanzania ni kubwa kuliko ile ya Kenya na Uganda taasisi hiyo imepanga kuziwezesha kwa kuzikopesha zaidi asasi na wadau wa nchini ili waweze kuhudumia kundi kubwa la watu kuliko ilivyo sasa ambapo nchi hizo zimekuwa zikipata fungu kubwa la fedha.

Kwa upande wake Katibu wa YWCA, Frida Mbowe alisema kwamba kwa kuwa manispaa hiyo inajiandaa kuwa hadhi ya jiji mkopo huo wa milioni 500/- utawawezesha kukarabati jengo kuwa lenye muundo wa kisasa utakaotoa mvuto kwa wawekezaji kupangisha na kufungua ofisi mbalimbali.

Naye Mbonea Maghimbi ambaye ni mwenyekiti wa Wazalendo aliishukuru Oiko Credit kuwakopesha bilioni 1.6/- na kusema watazitumia kama ilivyokusudiwa kwa kuwawezesha watu wa kipato cha chini kuweza kuinua hali yao kimaisha.

“Mbali na hilo pia tumepanga kuzitumia fedha hizo kutoa elimu kwa jamii inayotuzunguka umuhimu wa kujenga utamaduni wa kuhifadhi ama kujiunga na Saccos ya Wazalendo na faida mbalimbali watakazonufaika nazo mara watakapotimiza vigezo,” alisema Maghimbi.

Tangu Oiko Credit yenye makao makuu yake nchini Uholanzi ilipoanzishwa nchini mwaka 2006 imejiongezea wateja kutoka sekta mbalimbali ikiwemo benki, SME’s, Saccos, Makanisa na kuwekeza kutoka milioni 260/- hadi kufikia bilioni 16 Juni mwaka huu kutoka wateja wawili hadi 21

dr. bilal aendelea na ziara za kampeni mkoani iringa



Mgombea Mwenza wa urais wa kwa tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga, Dk. William Mgimwa, wakati alipofika katika jimbo hilo kufanya mkutano wa kampeni na kumnadi mgombea huyo leo.


Mgombea Mwenza wa Urais akiwaangalia wasanii wa Sarakasi wa Kikundi cha Kijiji cha Mabaoni Wilaya ya Mufindi, wakati alipokuwa akiwasili Kijijini hapo leo kufanya mkutano wa kampeni.


Wananchi wa Kijiji cha Mabaoni Kata ya Makungu Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa, wakimsikiliza mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa kampeni leo.

HOSPITALI YA REGENCY KUJENGA KITUO KIPYA CHA AFYA


Daktari Bingwa wa tiba za Mifupa, viuongo na upasuaji kutoka India Kaushal Mishra akizungumza na waandishi wa habari juu ya namna atakavyofanya kazi kwa kushirikiana na madaktari wa Hospitali ya Regeny.
Mwenyekiti wa Hospitali ya Regency Dr. Rajni Kanabar (kulia) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya uimarishaji na utoaji wa huduma za magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa ya mifupa na viungo, moyo, figo na magonjwa ya mfumo wa njia ya mkojo kwa kushirikiana na mataktari bingwa kutoka nchini India leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni meneja wa mifumo ya komyuta ya hospitali hiyo Jingne Oza.Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

Na Mwandishi Wetu.

UONGOZI wa Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam ,umesema unajenga kituo kikubwa cha afya kwa ajili ya kutoa huduma za afya chenye thamani ya dola za Marekani milioni 15 ili kupunguza gharama za wagonjwa wanaotibiwa nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa hospitali hiyo, Dk. Rajni Kanabar wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu ushirikiano wao wa kutoa tiba mbalimbali na kundi la madaktari bingwa kutoka India (Forts – Hospital Health Care Limited).

“Tumepata eneo jingine kwa ajili ya ujenzi wa kituo kikubwa katika eneo lililojirani na hospitali yetu, ambapo tunajenga mahabara ya kisasa na vyumba vya upasuaji viwili, sehemu ya huduma ya dharura na uongozi. Hivyo tumeshaanza ujenzi huo lengo ni kupunguza gharama kwa Watanzania kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya tiba mbalimbali,”

alisema.

Dk. Kanabar alisema ujenzi huuo untarajia kuchuku kipindi cha miaka miwili.

Akizungumzia kuhusu ushirikiano wa madaktari hao kutoka India, Dk. Kanabar alisema watakuwepo hapa nchini kwa kipindi cha miezi mitatu kwa ajili ya kutoa tiba na ushauri kwa wagonjwa ikiwemo kutoa mafunzo kwa madaktari wa hapa nchini, hata hivyo aliongeza baada ya muda huo kumalizika watakuja wengine.

Alisema uzinduzi rasmi wa ushirikiano huo, utazinduliwa Oktoba 16, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Madaktari hao, ni Dk. Rajesh KR. Pandit ambaye ni mtaalamu wa magonjwa ya moyo na Dk. Avinash Ingnatuius mtaalamu wa magonjwa ya figo ambao waliwataka Watanzania kufika hospitalini mapema ili kufanya matibabu kuwa rahisi badala ya kusubiri hadi wazidiwe.

Wengine ni Dk. Kushaul Mishra ambaye ni mtaalamu wa mifupa na viungo alisema wamefurahishwa kuja Tanzania. ambapo lengo lao ni kutoa ujuzi kwa madaktari waliopo nchini hususan namna ya kufanya upasuaji mgumu na Dk. Aman Gupta mtalaamu wa magonjwa yanatokana na mfumo wa njia ya haja ndogo.

Madaktari hao watatoa tiba hizo kwa gharama nafuu na kufanya upasuaji mdogo.

“Tutatumia kifaa kidogo kwa ajili ya kugundua matatizo ya mfumo wa haja ndogo ambacho hakiko Tanzania,” alisema Dk Gupta.

Hopitali ya Regency imetoa ufadhili kwa watoto zaidi ya 1,000 kwaa ajili ya upasuaji wa moyo kwa gharama ya dola za Marekani 1,650 hadi 2000

taasisi ya superbrands yaingia Tanzania


Mkurugenzi wa mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba na Mkurugenzi wa masoko Ephraim Mafuru wakionyesha cheti cha kudhibitishwa ubora wa kampuni na bidhaa zinazokubalika kwa wateja wa simu za mkononi afrika mashariki mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkurugenzi wa superbrands Jawad Jaffer(hayupo pichani)
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga akitoa shukrani mara baada ya kukabidhiwa cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi
Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries Limited Bw. Ajay Mehta akishukuru mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries Limited Bw. Ajay Mehta.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga ambaye aliambatana na Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mtahaba.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinazotambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru katikati ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi. Mwamvita Makamba.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Msaidizi wa Kampuni ya Azam Bw. Yusuph Kamau katikati ni Meneja Biashara wa kampuni hiyo ya Azam Bw. Daniel Hill aliyembatana nae.
Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer, akimkabidhi Cheti cha Superbrands inayothaminisha nembo ambazo zinatambulika na zenye viwango vya ubora wa juu zaidi Mkurugenzi wa Kampuni ya Chemi&Cotex Industies LTD, Bw. Lakshmi Narayan, Katikati ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Chemi&Cotex Industries LTD, Bw. Riyan Dewji. (Picha kwa hisani ya www.michuzijr.blogspot.com).

Sep 27, 2010

mbio za mashua bahari ya hindi zawa kivutio




Baadhi ya washiriki wa mbio za mashua za Vodacom Tanzacat wakishindana katika ufukwe wa bahari ya hindi yacht club ambapo zaidi ya boti 60 zilishindana na zaidi ya nchi kumi zilishiriki katika mashindano hayo ya kimataifa mashindano hayo yamefanyika kwa siku nne mfululizo.
Mwenyekiti wa Club ya Yacht Jim Bell(kushoto) akimkabidhi kombe mshindi wa mbio za mashua za Vodacom Tanzacat Blaine Dodds(kulia)wa pili kutoka kushoto ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza ,Peter Blaine

ridhiwani kikwete ndani ya chunya mkoani mbeya


Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM)Taifa,Ridhiwani Kikwete,akivishwa skafu alpowasili leo asubuhi katika Jimbo la Lupa, Chunya kuendeleza kampeni za ushindi wa kishindo kwa CCM.Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM)Taifa,Ridhiwani Kikwete, akiwatambulisha kwa wananchi, mgombea ubunge jimbo la Lupa, Victor Mwambalaswa kulia na mgombea Udiwani Kata ya Mbegani,Bosco Mwanginde leo asubuhi katika jimbo la Lupa,Chunya.Baadhi ya wakazi wa Kata ya Mbugani, Chunya wakisikiliza wakati Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM)Taifa,Ridhiwani Kikwete,akihutubia mkutano wa Kampeni uliofanyika katika Kata hiyo, Jimbo la Lupa, Chunya.

Sep 26, 2010

Wateja wa Vodacom sasa kuchati bure kwa Intaneti

· Ni kwa Face Book na nyinginezo

Dar es Salaam, 26 Septemba, 2010. Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua huduma mpya ya Intaneti ambayo itawawezesha wateja wake kuchati kwa intaneti bure.

Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi Mwamvita Makamba alisema jana kwamba wateja wa Vodacom sasa wanaweza kuchati bure kwenye tovuti za Face Book, the Grid na Vodamail.

Alisema Vodacom Tanzania inatoa huduma hiyo kwa lengo la kuwawezesha wateja wake kupata muda wa kuchati zaidi.

Alifafanua kwamba hayo yote yatawezekana kwa kutumia mtandao wa 3G ambao una kasi na nguvu kubwa.

“Tunapenda wateja wetu watumie mtandao wetu kwa kuwasiliana bure na hivyo kukata kiu yao ya mawasiliano”.

Alitoa wito kwa wateja wa Vodacom na Watanzania kwa ujumla kutumia huduma hiyo ya mtandao wa Intaneti.

Aliwaomba Watanzania kujiunga na Vodacom ili kupata huduma hiyo bure na hivyo kuwasiliana zaidi.

Alisema huduma hiyo itapatikana kwa simu za mkononi na pia kwa Laptop zilizounganishwa na USB Moderm.

Tangu kuanzishwa kwake miaka kumi iliyopita Vodacom imekuwa ikizindua huduma mpya kila mara kwa lengo la kurahisha huduma za mawasiliano kwa wateja wake.

Hivi sasa kampuni hiyo inawateja zaidi ya milioni saba ambao wanaunganishwa na huduma mbalimbali zenye lengo la kuboresha maisha yao, baadhi ya huduma hizo ni kama M-Pesa, ambayo ni njia ya haraka na uhakika ya utumaji wa pesa hapa nchini.

Vodacom ndiyo wa kwanza kuanzisha huduma hiyo hapa nchini.

ziara ya mama salma kikwete mkoani lindi

Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake WAMA Mama Salma Kikwete katika ziara yake ya uhamasishaji wanachama wa UWT Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kupiga kura wakati wa Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani oktoba 31 mwaka huu nchini Hapa likuwa akimnadi Mgombea ubunge Lindi mjini kupitia CCM Bw. Mohamed Abdulaziz.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimnadi mgombea Ubunge jimo la Mchinga Lindi vijjini Sulemani Mtanda
Mzuka unapopanda! mwachama wa UWT Lindi mjini akifurahia hotuba ya Mama Salma Kiwete wakati wa mkutano Lindi mjini
Umeyaona mambo ya vuvuzela! mwenye macho haambiwi tazama. hadi Lindi vijijini yapo pia.
Wanachama Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Lindi mjini wakimsikiliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati alipokuwa akiwahutubia.Picha na Mwanakombo Jumaa

dr. bilal mkoani kagera


Mgombea Mwenza wa Urais Kupitia tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimvisha kofia yake msanii mlemavu, Athuman Yunus, baada ya kufurahishwa na staili zake za uchezaji wa ngoma ya kabila la Kihaya, wakati wa mapokezi yake alipokuwa akiingia Kijiji cha Ruzinga Kanyigo Wilaya ya Misenyi Mkoa wa Kagera kufanya mkutano wa kampeni jana.
Mgombea Mwenza wa Urais Kupitia tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akifurahia staili za msanii mlemavu, Athuman Yunus, aliyekuwa akicheza ngoma ya kabila la Kihaya,wakati wa mapokezi yake alipokuwa akiingia Kijiji cha Ruzinga Kanyigo Wilaya ya Misenyi Mkoa wa Kagera kufanya mkutano wa kampeni jana.

Mke wa Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM Bi Zakia Bilal, akicheza wimbo wa kabila la Kihaya na Msanii Bahati Ibrahim, aliyekuwa akitoa burudani wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mayunga Mjini Bukoba jana .

Sep 25, 2010

Jk Aifunika musoma uwanja wa Mkendo!!

nMgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia maelfu ya wananchi wa Musoma Mjini kwenye mkutano mkubwa wa kampeni leo tarehe 25.09.2010
Malefu ya wakazi wa mji wa Musoma wakimkaribisha mjini Musoma mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipowasili katika viwanja vya Mkendo mjini Musoma na kuwahutubia katika mkutano mkubwa wa kampeni(picha na Freddy Maro)

Maalim Seif aahidi kupunguza kodi zanzibar


Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Ahmad


Na Mauwa Mohammed, Zanzibar

MGOMBEA wa urais wa Zanzibar, kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kama akichaguliwa kuwa rais wa Zanzibar, ataangalia upya viwango vya kodi ikiwa ni pamoja na kuvipunguza viwango vya ulipaji kodi ili kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara wengi zaidi.

Alisema utozaji kodi kwa kiwango kidogo kutawavutia wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza Zanzibar na kwamba uwekezaji huo pia utawanufaisha Wazanzibari wote tufauti na ilivyo hivi sasa ambapo wengine wamekuwa wakikwepa kuilipa.

Ahadi hiyo ameitoa leo hii alipokuwa akizungumza na wajasiriamali kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya Sunni Madrassa Mkunazini Mkoa wa Mjini Magharibi.

Alisema wafanyabiashara wadogo wadogo wanapaswa kusaidiwa na kuongezewa ujuzi ili waweze kuingia katika ushindani wa biashara ambapo Tanzania imeridhia kuingia kwenye soko la pamoja katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Nchi yoyote inayoendelea duniani, haiwakomoi wananchi wake katika kodi na badala yake inawawekea viwango vya chini, ili wazidi kuongezeka na mimi nitapunguza viwango vya ulipaji wa kodi kama mkinichagua kuingia ikulu,’’ alisema.

Maalim Seif, aliongeza kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa itakayoongozwa na CUF haitaruhusu wawekezaji matapeli wenye lengo la kunufaika kupitia migongo ya wananchi, bali itaruhusu wawekezaji ambao watainufaisha Zanibar na wananchi wake.

Alisema hawezi kuruhusu mtu kunufaika kwa gharama za Wazanzibari, lazima wawekezaji wenye tabia kama hiyo watawajibishwa kwani kuwaadhibu wananchi kwa kuwatetea wageni ni kosa na ni kuwadharau wananchi wazalendo.

“Mimi siamini kuwa kodi kubwa au utitiri ndio msingi wa maendeleo ya nchi, pia siamini kuwakamua wafanyabiashara wadogo wadogo ndiko kujenga nchi, naamini wafanyabiashara hawa wanatakiwa kusaidiwa ili wajiendeleze katika biashara zao,” alisema.

Aliongeza kuwa akiingia madarakani atahakikisha mafunzo kwa wajasiriamali yanatolewa kwa kiwango cha juu ili kuwajenga uwezo wa kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi kwa lengo la kukuza kipato chao.

Alisema wafanyabiashara wengi hususan wadogo wadogo wamekuwa wakifanya kazi zao kwa utundu, lakini wakipatiwa mafunzo watapiga hatua kubwa zaidi na taifa linanufaika.

DK. BILAL AVUNA KADI LUKUKI ZA WAPINZANI BUKOBA


Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM, Dr. Mohamed Gharib Bilal akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Mabila Wilaya mpya ya Kyelwa Mkoa wa Kagera, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kijijini hapo jana Sept 24 na kumnadi mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Rustas Katagila.
Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduxi CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipokea kadi za waliokuwa wanachama wa Vyama vya TLP, CHADEMA na CUF waliotoka katika Kata mpya ya Lukula, ambao walifika katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kijiji cha Mabila Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera jana Sept 23, ambapo jumla ya wanachama 144 kutoka vyama vya upinzani walitarajia kurejesha kadi zao na 14 kati yao walikabidhi kadi hizo kwa mgombea mwenza.

wanja la dr. kikwete na dr. bilal




Habari zenu Ndugu wapendwa,

Tunayofuraha kubwa kuwafahamisha ya kwamba tovuti maalumu na rasmi ya Mhe. Jakaya M. Kikwete na Dr. M. Gharib Bilal sasa inapatikana kwenye mitandao:


Tembelea tovuti hii maalumu ya Mgombea Uraisi na Mgombea Mwenza kwa tiketi ya CCM mwaka 2010 upate habari mbalimbali kama:

· Wasifu wa Wagombea – Mhe. Jakaya M. Kikwete na Dr. Mohammed Gharib Bilal.

· Mafanikio katika sekta mbalimbali.

· Sera na Malengo 2010 – 2015.

· Ratiba za kampeni.

· Hotuba maalumu.

· Matoleo ya Habari.

· Video na picha.

· Mitandao ya Facebook,Twitter na Youtube.

Kupitia tovuti hii na mitandao yake utaweza kupata taarifa mbalimbali na kutoa maoni yako.

“ PAMOJA TUZIDI KUSONGA MBELE”

Sep 24, 2010

P - FUNCK ATOA UFAFANUZI

P-Funk aka Majani ameizungumzia issue yake na Afande (Live kwenye Powerjamz Show - East Africa Radio) na kusema kuwa ni kweli Afande Sele alikua ana ngoma kwake lakini alikua hajamalizia kuilipia na jana ndio alikuja ghafla tena usiku na kuilipia but Afande alikua anaitaka fasta ili akai-release kwenye radio ila Majani alikua ana ratiba zake nyingine....So alikua hajambonji almost wiki nzima na alikua amekunywa dawa na kupumzika kidogo na ndipo Afande alipotinga na kutaka track yake ili akaiachie kwenye show. ......Kwa mujibu wa P-Funk sababu ya kumpiga "tena kibao tu" Afande ni kuwa alipotoka nje alimkuta Simba Dume akila "Cha Arusha" nje ya geti lake...na Majani ametamka kuwa hana noma wakae pamoja then wayamalize wala si lazima yafike "kwa kova"! KINACHOONEKANA HAPA NI KUWA HAKUNA BEEF,BALI NI LUGHA GONGANA TU BAINA YAO!
Kuna mtafaruku umetokea kati ya Afande Sele na Producer P-Funk wa Bongo Records mida hii ya mchana (Ijumaa) na Afande kupigwa na kwa mida hii amechukua RB kwa ajili ya kumfikisha Majani kwenye kwenye vyombo vya sheria. ......Ishu kwa mujibu wa Afande Sele ni hivi Afande alitoka Moro jana usiku akiwa na Ferooz na kumpatia Majani mkwanja kwa ajili ya kumalizia ngoma na kuambiwa aje leo (Ijumaa) kuchukua ngoma yake na alipofika kuchukua singo kwa mujibu wa Afande,Majani alimwambia yuko bize na kuanza kumpa kipondo!!!!(kwa hisani ya chini ya carpet blogspot.)

SERIKALI KUDHIBITI WAGANGA NA WAKUNGA WA TIBA ASILIA WANAKIUKA SHERIA!!

MAGRETH KINABO NA ARON MSIGWA- MAELEZO

SERIKALI imeagiza kuwa kila halimashuri ya wilaya,miji, manispaa na majiji iwe na Mratibu wa Tiba Asili ambaye atakuwa msimamizi wa masuala ya hayo, ikiwa ni hatua ya kuwadhibiti watoa huduma wa tiba hiyo watakaokiuka sheria.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni kwa niaba yake wakati uzinduzi wa usajili wa waganga wa tiba asili nchini.

“Mratibu huyu awe ni mfanyakazi katika idara ya afya aliyechini ya Mganga Mkuu wa Halimashauri husika,” alisema Waziri Mkuu Pinda.

Waziri Mkuu alisema hayo huku akiagiza kuwa waganga wanaofanya matendo yanayohatarisha uhai wa watu yanayohusisha waganga wa tiba asili ambayoni uuaji wa vikongwe, albino, watoto wadogo na uchunaji wa ngozi za binadamu kuwa hawatakuwa sehemu ya wizara hiyo.

“Yeyote atakayebanika kujihusisha na vitendo hivyo, wizara haitamtambua kuwa ni mganga na hivyo hatasajiliwa na kuruhusiwa kutoa huduma ya asili,” alisisitiza huku akisema waganga na wakunga na hasa waganga wa tiba asili nchini wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo yakiwemo maelekezo mbalimbali ya wizara hiyo.

Aliongeza kuwa waganga hao wanatakiwa kuanzisha vituo rasmi, kutoa huduma kwa mfumo wa kitaasisi na si mtu mmojammoja , kutayarisha dawa katika mazingira safi kujiendeleza kielimu na kuanzisha vitalu na mashamba ya miti dawa ili kuhifadhi dawa na mazingira ikiwemo kutunza kumbukumbu.

Akizungumzia kuhusu usajili huo, Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Deo Mutasiwa alisema waganga na wakunga wa tiba asili wataruhusiwa kusajiliwa kwa mujibu wa sheria namba 23 ya mwaka 2002 na kanuni zake. Hivyo watakaokiuka wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

Dk. Mutasiwa aliongeza suala la usalama wa dawa za tiba hizo litasimamiwa na Serikali chini , Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA), lakini la kuhusu jukumu la dawa na jinsi inavyofanya kazi litakuwa na mwenyewe dawa .

Na Mwakilishi Shirika la Afya Duniani Tanzania (WHO) Dk. Rufaro Chatora, alishauri wanasayansi kufanya utafiti wa dawa za asilia ili kuboresha huduma hiyo. Pia utafiti wa dawa hizo ukishirikisha na ule dawa za kisasa ufanyanyike ili kuimarisha na kuendeleza huduma hizo kwa kisasa.

AFANDE ACHEZEA KICHAPO TOKA KWA MAJANI


Kuna mtafaruku umetokea kati ya Afande Sele na Producer P-Funk wa Bongo Records mida hii ya mchana (Ijumaa) na Afande kupigwa na kwa mida hii amechukua RB kwa ajili ya kumfikisha Majani kwenye kwenye vyombo vya sheria. ......Ishu kwa mujibu wa Afande Sele ni hivi Afande alitoka Moro jana usiku akiwa na Ferooz na kumpatia Majani mkwanja kwa ajili ya kumalizia ngoma na kuambiwa aje leo (Ijumaa) kuchukua ngoma yake na alipofika kuchukua singo kwa mujibu wa Afande,Majani alimwambia yuko bize na kuanza kumpa kipondo!!!!

P.Funk kapigiwa simu now ikiwa ONLINE East Africa Radio na kusema kuwa amelala wampigie baadae, na nia yakumpigia ni kwamba walitaka kujua upande wa pili wa P.Funk.
(Kwa niaba ya NAY WA MITEGO aliyeshuhudia chezo pale bongo recordz)

NITATEKELEZA ILANI YA CCM KWA KASI ZAIDI, NGUVU ZAIDI NA KUWAPA VIJANA AJIRA,MO DEWJI…!!!

MO akihutubia wananchi wa Kata ya Unyambwa.

*******************

Na Hillary Shoo.

Singida. Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM, Mohamed Gulam Dewji, amesema endapo wananchi watampa ridhaa ya kuendelea kuwawakilisha tena bungeni, atatekeleza Ilani ya CCM kwa kasi zaidi ikiwemo kutafuta ufumbuzi wa namna ya kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana.

Dewji alisema katika ilani uchaguzi, CCM imeainisha wazi kwamba inatambua tatizo la ajira na hasa ajira ya vijana wanaomaliza elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu kila mwaka kuwa, ni kubwa mno.

“Vijana hawa wote ni nguvu kazi ya taifa ambayo inaweza kutumika katika kazi na shughuli halali za ujenzi wa nchi yetu na ikapiga hatua kubwa ya kimaendeleo”,alisema Dewji.

Mgombea huyo,alisema ili kukabiliana na tatizo hilo, CCM ina mpango wa kupanua mafunzo ya VETA yaweze kuchukua vijana wengi zaidi, ili waandaliwe kujiajiri wenyewe.

Aidha, alisema vijana watahamasishwa kuanzisha miradi ya kiuchumi na kujiunga katika vikundi vya ushirika vya kuweka na kukopa (SACCOS) ili waweze kupata mikopo kwa masharti nafuu.

“Katika miaka mitano iliyopita, nimewatafutia kazi vijana kutoka jimboni kwetu kwenye kiwanda changu cha nguo cha Afritex kilichopo mkoani Tanga., Kuajiri vijana hao, nimefanikiwa kwa kiasi fulani kupunguza idadi ya vijana wetu wanaomaliza elimu ya sekondari, kukaa vijiweni”,alisisitiza huku akishangiliwa na mamia ya wananchi.

Dewji aliyasema hayo jana katika mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Unyambwa.

Wakati huo huo,Dewji alitumia fursa hiyo kumwombea kura mgombea urais Jakaya Kikwete kwa madai kwamba ameonyesha uwezo mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa ilani za uchaguzi. Aidha, alimnadi mgombea wa udiwani wa kata hiyo, ya Unyambwa Salum Satu na kuomba apewe kura za kutosha kumwezesha kushika nafasi hiyo.

MO, akisistiza kuwa Katika kipindi cha miaka saba michezo imeweza kupaa katika mkoa wa Singida ambapio Kindai Shooting Stars, timu ya mkoa ilibeba kombe la kilimanjaro Taifa Cup kwa mara ya kwanza katika historia ya mkoa huo.

MO akizcheza ngoma ya Kinyaturu ya kutikisa mabega, maarufu kwa jina la tikisa mabega tingisha kiuno.

Wanafunzi wa shule ya msingi Unyambwa wakimpokea MO kwenye viwanja vya shule hiyo wakati alipokwenda kweye mkutano wa kampeni wa Kata hiyo.

Wanafunzi wakiwa na mabango yanayomnadi MO huko KatikaKata ya Unyambwa.

Visura 10 kuonesha mavazi yaliyooneshwa na Mustafa Hassanali nchini Cameroon February na Zanzibar Julai 2010.

Mwanzilishi na muandaaji wa jukwaa la wanawake wajasiriamali Tanzania (TWENDE ) na Jukwaa la kukuza vipaji vya wabunifu chipukizi Swahili Fashion Week, ambae pia ni mbunifu maarufu wa mavazi, Mustafa Hassanali amealikwa kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya mavazi yanayofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku mbili tarehe 23 na 24 ya mwezi huu katika hoteli ya New Arusha.

Maonyesho hayo yameandaliwa na Maridadi. Maridadi ni kikundi kinachojumisha wanawake watatu kutoka mataifa tofauti ya Tanzania, Austarialia na Uholanzi ambao wanaishi nchini katika jiji la Aruha na kujishughulisha na masuala mbalimbali yanayohusiana na mendeleo ya mwanamke..

Akielezea lengo la kuandaa maonyesho hayo, mmoja wa wanawake hao, Lilian Bulengo

amesema kuwa “dhumuni kuu la kuandaa tukio hili linalojulikana kwa jina la “Maridadi Women Show” ni kuwakutanisha pamoja wanawake kutoka maeneo tofauti ya Arusha na Moshi katika Fashion Show, maonyesho ya biashara pamoja na kupata fursa ya kuzungumza mambo mbalimbali yanayowakabili wanawake katika maisha ya kila siku hapaTanzania ikiwemo suala la unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji, wanawake na kuondokana na utegemezi na masuala ya uchumi na biashara kwa ujumla”.

Mustafa Hassanali, pamoja na kuwa mgeni rasmi, pia ataonyesha mavazi ambayo kwa mara ya kwanza alionyesha nchini Cameroon mezi wa 2 mwaka huu katika show iliyojulikana kama PARFUM D’AMOUR, na mavazi yanayojulikana kwa jina la Karafuu collection aliyoyaonyesha julai 2010 Zanzibar.

Jumla ya visura 10, kati yao nane kutoka Dar es salaam na wawili kutoka Arusha watapita jukwaani na kuonyesha mavazi hayo ya Mustafa Hassanali, ambayo yanawavutia wengi kutoka na ubunifu wa hali ya juu.

“Nimefurahi sana kupata fursa ya kuwa mgeni rasmi katika tukio hili, pia kuonyesha nguo zangu ambazo zilipendwa sana Cameroon, naamini pia wakaazi wa Arusha watafurahia kazi yangu” . Alisema Hassanali.

Katika maonyesho haya Mustafa ataonyesha na wabunifu wengine kutoka Arusha ambao ni Shwari Collectables,Hanifa Hash na Woolworth.

Mbali na maonyesha hayo pia siku ya jumamosi kutakuwa na manyesho ya kibiashara yatakayojumuisha kazi mbalimbali za sanaa za mikono. Benki nazo zitapata fursa ya kuonyesha na kuelezea shughuli zao mbalimbali wanazozifanya hasa katika kuchangia maendeleo ya wanawake Tanzania.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA