Sep 13, 2010

hivi ndivyo ilivyokuwa miss tz bongo

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom,Dietlof Mare (kushoto) akikabidhi funguo ya gari aina ya Hyundai i10 kwa mrembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel mara baada ya kunyakua taji la urembo huo usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar.
Vodacom Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel (kati) akiwa na mshindi wa pili Glory Mwanga (kushoto) na Consolata Lukosi.
AY stejini.
THT.
Vodacom Miss Tanzania aliemaliza muda wake,Miriam Gerald (shoto) akimvisha taji Vodacom Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel mara baada ya kutangazwa mshindi wa taji hilo usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Mlimani City.
Mwakilishi wa Bodi ya Utalii,Dr. Aloyce Nzuki akikabidhi taji kwa mshindi wa Utalii,Salma Mwakalukwa.
shamra shamra wakati wa kutangazwa kwa mshindi wa Vodacom Miss Tanzania 2010.
Meneja wa Bia ya Redd's,Kabula Nshimo (shoto) akiwa na Balozi wa Redd's,Consolata Lukosi mara baada kumtangaza.
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Prashant Patel akitangaza wa Mrembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010,katika ukumbi wa Mlimani City usiku wa kuamkia leo.
Majaji wakipitia majina ya warembo kabla ya kuyatangaza.
tano bora.
kumi bora.
MC Taji Liundi akiwa amezunguwa na warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010,wakati akimkaribisha Mratibu wa Majaji,Dr.Ramesh Shah aje kutangaza kumi bora ya warembo hao.
baadi ya warembo wakipita kujionyesha kwa wadau wa urembo waliofika katika ukumbi wa Mlimani City usiku wa kuamkia leo.
Warembo wakipita na vazi la Beach.
Msanii wa Bongo Freva,Mwasiti akiwa na vijana wa THT wakifanya vitu vyao.

Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakionyesha shoo yao ambayo ilipendeza na kuvutia sana.
Wasanii wa Bongo Freva toka TMK,Mh. Temba (shoto) na Chege walipagawisha vilivyo ndani ya ukumbi wa Mlimani City usiku wa kuamkia leo.
Msanii Wahuu toka Kenya nae hakuwa nyuma katika kutoa burudani kwa wadau wa urembo waliofika Mlimani City usiku wa kuamkia leo.
Mzee wa Kiduku,Mataluma nae hakuwa nyuma katika burudani.
TMK wanaumeeeee.........
Ma MC wa shughuli hiyo,kulia ni Taji Liundi na Jokate Mwegelo.
Mie nikiwa na wadau toka shoto ni Mrembo alieshiriki Miss Tanzania 2009,Sylvia Sharry,Martin pamoja na Mwanamitindo Maarufu nchini,Mustafa Hassanali.
Waheshimiwa,kulia ni Waziri wa Nishati na Madini,Mh. William Ngeleja akiwa na mkewe,Pia Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam,Mh. William Lukuvi na mkewe wakifuatilia kwa makini mashindano hayo.
Wadau wa TBL
wageni mbali mbali walihudhulia katika mashindano hayo ya urembo.

Sep 11, 2010

GENEVIVA MPANGALA NDIYE VODACOM MISS TANZANIA 2010!!

Vodacom Miss Tanzania Geneviva Mpangala akiwa na washindi wenzie mara baada ya kutangazwa mshindi kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam usiku huu kulia ni mshindi wa tatu Consolata Msofe na kulia ni mshindi wa pili Groly Mwanga, Geneviva ataiwakilisha nchi katika shindano kubwa la Dunia Miss World litakalofanyika mwishoni mwa mwaka huu. Katika shindano hilo wanamuziki mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya wamefanya vitu vyao wakiwemo Temba na Chege kutoka TMK Family, Ambwene Yessaya (AY) Mataluma, Mwasiti na kundi la THT kutoka jijini Dar es salaam na wengine wengi.
Hii ni Tano Bora ya Vodacom Miss Tanzania mara baada ya kutangazwa ambapo waliulizwa maswali na kuyajibu kabla ya kutangaza mshindi wa shindano hilo kwa mwaka huu wa 2010.
Hii ndiyo kumi bora ya Vodacom Miss Tanzania mara baada ya kutangazwa kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam usiku huu.
Washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania wakipita jukwaani na vazi la ufukweni ilikuwa si mchezo.
Utambulisho
Utambulisho
Warembo wakipita na kujitambulisha kwa wageni waalikwa na mashabiki wa urembo.
Wakuu wa Kampuni ya MUZASHA TOURS wakishuhudia shindano hilo kulia ni Benedictor Mulokozi Mkurugenzi wa CM Co. Limited Charles Mtawali Mkurugenzi wa MUZASHA TOURS Muzamir Katunzi pamoja na Pamela ambaye ni maiwaifu wa Charles Mtawali.
Warembo wanaoshiriki kwenye shindano la Vodacom Miss Tanzania wakiingia kwa shoo ya utambulisho.
Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam William Lukuvi aliyekaa chini pamoja na Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dk Ladslaus Komba akiingia na ujumbe wake kutoka Bodi ya Utalii na Mamlaka ya hifadhi za Ngorongoro kabla ya kuanza kwa shindano hilo huku akisindikizwa na Mkurugenzi wa Kamti ya Miss Tanzania Hashim Lundenga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare akihojiwa na mtangazaji wa Star Tv kabla ya kuanza kwa shindano hilo.
Warembo wakiingia kwenye ukumbi wa Mlimani City tayari kwa kupanda jukwaani.

SAFIRI SALAMA P.DIDY

Ile safari ya mwisho ya kila binadamu katika duniani hii kwa Perfect kasiga 'P. Diddy' imehitimishwa jioni ya leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam huku warembo kibao wakipoteza fahamu wakati wa kuaga mwili wake. Ibada ya kumuombea marehemu, ambaye alikuwa mchumba wa mtangazaji wa TBC1, Maimartha Jesse, ilifanyika nyumbani kwake Kinondoni kwa Mwanamboka. P. Diddy, alifariki dunia ghafla barabarani mtaa wa Lumumba jana jijini Dar es salaam na kifo chake kushitua wadau wengi wa burudani jijini Dar es salaam.

Mtangazaji wa wa kipindi cha B&M, Ben Kinyaiya, ambaye anafanyakazi pamoja na Maimartha, mchumba wa marehemu, akitoa salamu zake za mwisho mbele ya jeneza huku akilia.

..hakika ni wakati wa majonzi na kilio kwa Ben Kimyaiya.

...warembo waliofanyakazi pamoja na marehemu katika masuala ya burudani walishindwa kujizuia kulia kwa uchungu


'Kimwana wa Manywele' (kati) ambaye anashikilia taji hilo lililoandaliwa na marehemu enzi za uhai wake, alikuwa miongoni mwa warembo waliopoteza fahamu (pichani chini) baada ya kumuaga marehemu.


Judith Mosha akisaidiwa kutembea baada ya kumuaga marehemu. Judith ndiye Mkurugenzi wa bendi ya Diamond Musica ambayo marehemu alikuwa mkurugenzi msaidizi wake ambaye alipanga bendi yake ifanye shoo kabambe wakati wa sikukuu ya Idd leo.

baadhi ya wanamuziki wa bendi waliohudhuria maziko....akiwemo Ali Choki (shoto), Kalala junior (wa pili kulia)

Maimartha Jesse akibebwa kuingia makaburini baada ya kushindwa kutembea.


MUNGU ALITOA NA MUNGU AMETWAA MJA WAKE, AILAZE ROHO YA MAREHEMU PEPONI-AMEEN!

(msaada toka global publisher)

TIP TOP NAO WAKATUPIA BADO TUNAPANDA KWA SOKO AISEE!!

Deso

Jana usiku vijana kutoka Tip Top Connection walizindua album yao inayoitwa Bado Tunapanda, uzinduzi ulikwenda vizuri sana na wasanii walioisindikiza show hiyo walifanya vizuri sana wakiwemo Lina, Yung D, Godzilla, Jafaray, Roma na Mwasiti.

FM ACADEMIA WAZINDUA "VUTA NIKUVUTE" KWA KISHINDO DIAMOND JUBILEE USIKU HUU!!

Mkurugenzi wa Mabibo Heineken Beer Benedicta Rugemalila kulia akipunga mikono mara baada ya kuizindua albama ya sita "Vuta Nikuvute" ya Bendi ya muziki wa dansi FM Academia kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu akishirikiana kwa pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa Zain Kelvin Twisa wa pili kutoka kulia na Felician Mutta katikati, anayeonekana kuzungumza ni MC wa shughuli hiyo Benny Kinyaiya.
Rais wa Bendi ya FM Academia Nyoshi El Sadaat wa pili kutoka kushoto akiongoza wanenguaji wa kiume kutoka bendi hiyo wakati walipopanda jukwaani kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, FM Academia wanazindua albam yao ya sita inayoitwa "Vuta Nikuvute" usiku huu. Kumekuwepo na burudani mbalimbali kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee unaojumuisha wanamuziki mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania, ambapo mwanamuziki Nameless kutoka nchini Kenya amefanya mambo makubwa huku akishangiliwa na mashabiki waliohudhuria kwenye uzinduzi huo.
Watotowazuri kutoka Bendi ya FM Academia waliendelrea kukonga nyoyo za mashabiki kwa staili mbalimbali wakati walipokuwa walionmyesha Makeke yao jukwaani.
Vimwanba wa FM Academia wakifanya vitu vyao jukwaani ilikuwa ni shoo babkubwa.
MC wa shughuli hiyo Benny Kinyaiya ambaye ni mtangazaji wa TBC1 akizungumza wakati alipokuwa akiendesha utaratibu wa onesho hilo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu.
Mwanamuziki Nameless akimbembeleza kwa sauti nzuri huku akiwa amepiga magoti mmoja wa mashabiki wakati alipokuwa akiimba kwenyer ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu.
Mwanamuziki Nameless kutokam Kenya akimchukua mmoja wa mashabiki wa muziki waliohudhuria kwenye uzinduzi wa albam ya Bendi aya FM Academia ili wacheze wakati mwanamuziki huyo alipokuwa akitumbuiza kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu.
Mmiliki wa Bendi ya FM Academia Martin Kasyanju katikati akimtambulisha Felician Mutta kushoto kwa Mkurugenzi Masoko wa Zain Kelvini Twissa.
Mashabiki na wageni mbalimbali walioalikwa katika uzinduzi huo unaofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu.
Mmiliki wa bendi ya FM Academia Martin Kasyanju kulia akiwa pamoja na mmiliki wa zamani wa bendi hiyo Feliciani Mutta anayefuata akiwa ameongozana na maiwaifu wake kushoto ni Mkurugenzi wa Mabibo Heinekein Beer mama Benedicta Rugemalila wakiwa katika uzinduzi huo.

Sep 10, 2010

WAGOMBEA UBUNGE WATAMBULISHWA UBUNGO NA KAWE!!

Mgombea Ubunge (CCM)jimbo la Kawe Angela Kizigha (kulia) akiomba kura mbele ya mama Salma Kikwete kwa wapiga kura wake jijini jana uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika oktoba 31 mwaka huu nchini kote.
Baadhi ya Madiwani Wanawake jimbo la Kinondoni na Ubungo Mkoa wa DSM wakitambulishwa na kuombewa kura katika uchaguzi Mkuu ujao.
Kijana ambaye kura zake hazikutosha katika kura za maoni Nape Mnauye (kulia) akiongea katika mkutano wa umuhimu wa kupika kura.
Kinamama wa UWT wa Jimbo la Kinondoni na Ubungo wakishangilia wakati wa utambulisho wa wagombea ubunge wa Ubungo na Kinondoni

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA