Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Sep 4, 2010
TAIFA STARS YAWIKA MBELE YA WAARABU WA ALGERIA NA KUTOKA SARE 1-1!!
WAREMBO VODACOM MISS TANZANIA KULAMBA MILIONI 46.6
Warembo wakiwa katika ushiriki wa kutafutwa balozi wa redd's
Mh. Kikwete Aiteka Kawe, Ubungo na Mbagala leo
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Mh. Dr. Jakaya Kikwete akihutubia wana CCM wa jimbo la Ubungo,katika ukumbi wa Ubungo plaza,jijini dar leo.
wana CCM wa jimbo la kawe wakimsikiliza Mh. Dr. Jakaya Kikwete ukumbi wa Ubungo plaza
Mwana CCM akitoa hoja ukumbi wa Nakiete, Mbezi Beach, wakati Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Mh. Dr. Jakaya Kikwete alipokutana na wanachama wa jimbo la Kawe na kuwahutubia leo.
Mh. Dr. Jakaya Kikwete akihutubia uwanja wa wana CCM na wapenzi wa chama hicho katika viwanja vya Zakheem, Mbagala jijini dar leo
Kadi za chama cha CUF zikionyeshwa kwa Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM mara baada ya wenye nazo kiasi cha 80 hivi kuamua kurejea CCM.
Wanachama wapya wa CCM wakila kiapo baada ya kutoka CUF uwanja wa Zakheem, Mbagala leo.
Shamrashamra za kumkaribisha Mh. Jakaya Kikwete katika viwanja vya Zakheem,Mbagala alipokwenda kwa ajili ya kuinadi ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) na kuwahutubia leo.
Umati wa wana CCM na wapenzi wa chama hicho wakiwa wamefutika katika uwanja wa Zakheem Mbagala leo kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais kwa tikweti ya CCM,Mh. Dr. Jakaya Kikwete.
wana CCM wengi walijitoteza katika viwanja vya Zakheem,Mbagala leo.
Sep 3, 2010
MKURUGENZI WA MAENDELEO WIZARA YA HABARI AWAFUNDA WAREMBO VODACOM MISS TZ!!
Baadhi ya Warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni wa Wizara ya Habari utamaduni na Michezo Hermas Mwasoko. wakati alipowatembelea kambini kwao katika Hoteli ya giraffe DAR ES sALAAM.
WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AHUDHURIA MKUTANO WA MAPINDUZI YA KILIMO GHANA!!
AY achaguliwa kushiriki tuzo nchini ufaranza,watanzania tumpigie kura ili aweze kushinda
Sasa amechaguliwa katika final za Tuzo za Ufaransa za RADIO FRANCE INTERNATIONALE DISCOVERIES AWARD 2010 {Rfi Prix Découvertes 2010} zitazofanyika September,ndani ya Paris.
AY anawaomba watanzania wote kumpigia kura za kutosha aweze/tuweze kushinda tuzo hizo.Unaweza kuvote kupitia
www.rfimusique.com
PAMOJA SANA
Dr. Bilal Akiwa Mjini Songea
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi,Dk. Mohamed Gharib Bilal, akifurahia vazi la asili ya kabila la Wangoni na silaha ya Kinjenje, baada ya kukabidhiwa na wazee wa kabila hilo, Aidan Mbano (kushoto) na Joachim Silo, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Bombambili mjini Songea jana.
Mgombea Mwenza wa Urais,Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi Mgombea wa ubunge wa jimbo la Songea mjini, John Nchimbi, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Bombambili mjini Songea
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal, akishuka jukwaani na vazi la asili la kabila la Wangoni na silaha ya Kinjenje aliyokabidhiwa na Wazee wa Kabila hilo ili kujilinda na wabaya wake wakati wa mapigaino, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Bombambili mjini Songea jana
Dk. Mohamed Gharib Bilal, akivishwa vazi la asili la kabila la Wangoni na wazee wa kabila hilo, Aidan Mbano (katikati) na Joachim Silo, wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Bombambili mjini Songea
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Songea Mjini, John Nchimbi, (wapili kushoto) akimkaribisha mgombea Mwenza wa Urais kwenye jimbo lake katika Uwanja wa Bombambili wakati alipofika kufanya mkutano wa kampeni. Kushoto ni mgombea ubunge wa Viti maalum wa Mkoa wa Ruvuma, Devotha Likokola.
Dk Mohamed Gharib Bilal na mkewe Bi. Asha Bilal, wakiangalia ngoma ya Ligambuza ya kabila la Wangoni, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Bombambili mjini Songea kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni na kuinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi
Mgombea Mwenza wa Urais,Dk. Mohamed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Shina la wakereketwa la CCM Stand Mpya lililopo katika Jimbo la Peramiho Wilaya ya Songea Mjini. Kulia ni Mgombea ubunge wa jimbo hilo,Jenista Mhagama.
Wananchi wa Wilaya ya Songea mjini,wakiimba na kumshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akiingia kwenye Uwanja wa Bombambili kuhutubia wananchi katika mkutano wa kampeni, ikiwa ni pamoja na kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo hilo John Nchimbi.Picha na Muhidin Sufiani.