Aug 31, 2010

Designers visiting the Textile Sector Development Unit


Designers being shown the Modern industral Patern cutter BY PRODUCTION MANAGER PATRRICK LUMUMBA.
Designers Kemi Kalikawe , Manju Msitta and Ailinda Sawe seeing how a machine operates.
Designer listening to Patrick Lumumba of the Production Facility they Visited on 30 September 2010.
Designers attending to how the pattern drafting works

Dr. Bilal Aendelea na ziara ya kampeni masasi na nayumbu!!!


Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Bilal akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Nanyumbu baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Masasi leo
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab akimvisha skafu Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala leo mchana
Mgobea Mwenza wa urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Masasi, baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Newala, leo
Baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Newala Mkoa wa Mtwara, wakiwa katika magari kwenye msafara wa kumsindikiza Mgombea Mwenza wa nafsi ya urais, Dk Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akitoka Wilaya hiyo kuelekea Wilaya ya Masasi leo asubuhi
wananchi wa Kijiji cha Lukuledi Wilaya ya Masasi Mkoa wa Mtwara, waliojitokeza kumsikiliza mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia na kuwanadi wagombea Ubunge wa Jimbo la Lulindi,Bwanausi Dismas na Mariam Kasembe wa Jimbo la Masasi leo
Wananchi wa Kijiji cha Mangaka Wilaya ya Nanyumbu Mkoa wa Mtwara Jimbo la Nanyumbu, wakimsikiliza mgombea mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Kijiji hicho leo mchana.

(Picha na Muhidin Sufiani)

tano Wa Marais Wastaafu Wafanyika Jijini Dar


Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi (katikati) akiongea na washiriki wa mkutano unaowahusisha marais wastaafu wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni balozi Charles Stith ambaye pia ni mkurugenzi wa kuhifadhi kumbukumbu za marais wa Afrika.
Baadhi ya viongozi wastaafu wa nchi za Afrika na wale walioko madarakani wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa ufunguzi wa mkutano unaowahusisha marais wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Rais mstaafu wa Jamuhuri ya Mauritius, Dkt. Kenneth Kaunda rais mstaafu wa Zambia, Waziri mkuu wa sasa wa Msumbiji Bi. Luisa Diogo na Waziri mkuu mstaafu wa Tanzania Fredrick Sumaye. Washiriki wa mkutano wa marais wastaafu wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani kutoka nchi mbalimbali za Afrika na vyuo vikuu kutoka ndani na nje ya Afrika wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa wakati wa mkutano wa marais wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam.
(Picha na Aron Msigwa)

Aug 29, 2010

Chama cha NCCR Mageuzi chazindua ilani yake ya uchaguzi

Pichani ni mgombea urais kwa Chama cha NNCR Mageuzi, Hashim Rungwe akionyesha ilani ya uchaguzi ya chama hicho wakati wa uzinduzi wa kampeni ya chama hicho leo jijini Dar. CHAMA cha NCCR Mageuzi leo kimezindua ilani yake ya Uchaguzi huku kikitaja mambo 12 ambayo chama hicho kitaelekeza nguvu iwapo kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi.Wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa chama hicho taifa James Mbatia alisema chama chake kitazindua kampeni zake kitaifa Septemba 11 baada ya mfungo wa ramadhani ili kutowakwaza Waislam ambao wako kwenye mfungo wa mwezi mtukufu.“Ajenda yetu kuu itakuwa ni katiba, tumeainisha mambo yatakayokuwemo kwenye katiba hiyo, hili ndilo nataka wagombea wetu mlizungumzie kwa kina,” alisema Mbatia.

VODACOM YAFUTURISHA PANGANI NA KUGAWA MISAADA YA CHAKULA KWENYE MADRASA!!

Mwamvua Mlangwa Mratibu wa Uhusiano Vodacom Foundation kulia akikabidhi madaftari kwa watoto wa mji Vituo vya watoto yatima na Madrasa mbalimbali Pangani. mara baada ya kufuturu katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation, wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kushoto ni, Sheikh Mohamed Khalili Mwakilishi kutoka Tanga mjini, Sheikh Khamis Rashid mwakilishi wa Sheikh wa Pangani na Grace Lyon Afisa Vodacom Foundation.

Mtoto Bwaga Abdallah akipokea mfuko wa sukari kutoka kwa Maafisa wa Vodacom Foundation Grace Lyon kulia na Mwamvua Mlangwa wa pili kutoka kulia huku akisaidiwa na Sheikh Mohamed Khalili kushoto kutoka Tanga mjini na Sheikh Khamis Rashid Mwakilishi wa Sheikh wa Pangani wa pili kutoka kushoto, katika msaada huo pia Vodacom Foundation iligawa Mchele, Maharage, mafuta ya kula pamoja na vifaa vya shule.

: wakazi wa mji wa Pangani waliojitokeza katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation wakisubiri muda ufike ili waweze kufuturu Vodacom Foundation pia iligawa misaada ya Mchele, Mafuta ya kula, maharage na vifaa vya shule kwa watoto wa Dadrasa mbalimbali na vituo vya watoto yatima mjini Pangani
Wakazi wa mji wa Pangani wakipata futari mwishoni wa wiki ambapo Vodacom Foundation iliwafuturisha na kugawa vyakula na vifaa vya shuleni wa watoto yatima na madrasa mbalimbali mjini humo ambavyo ni Mchele, maharage, mafuta ya kula, sukari na vifaa vya shuleni kwa ajili ya wanafunzi.
Wakazi wa mji wa Pangani wakipata futari mwishoni wa wiki ambapo Vodacom Foundation iliwafuturisha.

CUF wazindua kampeni zaao


Mwenyekiti wa CUF na mgombea urais wa chama hicho cha wananchi, Prof. Ibrahim Lipumba akisalimia wanachama wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya chama hicho katika viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar
Prof. Lipumba akisalimiana na Mh. Hamad Rashid mmoja wa wanachama na viongozi waandamizi wa CUF.
Sehemu ya umati wa wana CUF mkutanoni hapo

Rais Kikwete Awasili Mkoani Mbeya


Rais Jakaya Kikwete akihutubia umati wa wakazi wa Tunduma jioni hii wakati akianza kampeni yake mkoa wa Mbeya.
Rais Jakaya Kikwete akihutubia jioni hii mjini Tunduma ambako kumetia fora sana kwa umati mkubwa wa watu katika vituo vidogo vya mikutano ya kampeni za Chama tawala CCM
Uwanja wa mkutano Tunduma ulikuwa hautoshi
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mark Mwandosya akimfagilia njia JK ya kuhutubia wananchi wa Tunduma leo

Dr.Bilal aendeleaa kuinadi ilani ya CCM mkoani mtwara


Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Kijiji cha Ntiniko Wilaya ya Mtwara Vijijini Mkoa wa Mtwara.
Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal akipita katikati ya chipukizi baada ya kupokelewa katika mpaka wa Wilaya ya Mtwara Mjini na Tandahimba Mkoa wa Mtwara wakati akiwa kwenye ziara yake ya mikutano ya kampeni leo mchana.
Mgombea Mwenza wa nafasi ya urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Nanguruwe Wilaya ya Mtwara Vijijini baada ya kusimama eneo hilo wakati akielekea Kijiji cha Ntiniko katika mkutano wa kunadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo.
Wananchi wa Kijiji cha Nahyanga Wilaya ya Tandahimba Mkoa wa Mtwara, wakimsikiliza Mgombea mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal wakati wa mkutano wa kampeni.

Rais Kikwete apokelewa kwa shangwe sumbawanga na mpanda


Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Kikwete akimnadi kwa wananchi mgombea Ubunge wa jimbo la Sumbawanja mjini kupitia chama hicho,Bw.Khalfan Hayeshi pindi alipokuwa katika mkoa wa Rukwa jana.
Rais Jakaya Kikwete akigombewa kusalimiwa na wananchi wa Sumbawanga alipokuwa akiwasili katika uwanja wa Mandela.
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi pindi alipowasili mjini Mpanda na kufanya mkutano wa kampeni.
Rais Jakaya Kikwete akishuka kwenye Helkopta mara baada ya kuwasili Sumbawanga mjini tayari kwa mkutano uliofanyika jana kwenye uwanja wa Mandela.
Wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akihutubia.

Wanachi wa mji wa Sumbawanga wakiwa wamefurika ndani ya Uwanja wa Mandela kumsikiliza Rais Jakaya Kikwete wakati akiwahutubia.

Warembo wa Miss Tanzania watembele mapango ya amboni tanga


Baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010, wakisikiliza maelezo ya historia ya Mapango ya Amboni Mkoani Tanga jana wakati warembo hao walipotembelea eneo hilo ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii Kanda ya Kaskazini na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.
Warembo wa Vodacaom Miss Tanzania 2010 wakipita katika mapango ya Amboni mkoani Tanga jana kujionea maajabu mbalimbali ya maopango hayo wakati wa ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo Kanda ya Kaskazini ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii Kanda ya Kaskazini na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.
Warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakipiga picha na watoto waliotembelea mapango ya Amboni mjini Tanga jana ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii Kanda ya Kaskazini na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

Aug 28, 2010

RAIS JAKAYA AWASILI MPANDA TAYARI KWA KAMPENI!!

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akimsalimia mtoto ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja muda mfupi baada ya mgombea huyo kuwasili katika uwanja wa michezo wa mjini Mpanda ambapo alihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni leo mchana.
Baadhi ya wakazi wa mji wa Mpanda wakimkaribisha kwa mabango mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, Dr.Jakaya Mrisho Kikwete jana mchana.(picha na Freddy Maro)

Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA mama Salma Kikwete ziarani mkoani Mbeya!!

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti waUWT mkoa Dodoma Fatma Tawfiq Agosti 28,2010 alipowasili katika uwanja wa ndege Mkoa wa Mbeya .(kati )ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya James Msekela. Picha na Mwankombo Jumaa-MAELEZO.

Kikundi cha ngoma ya asili cha wakina mama mkoani Mbeya kikimtumbuiza Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) alipowasili (Agosti 28.2010) katika uwanja wa ndege wa Mkoani Mbeya katika muendelezo wa ziara zake za kuwahamasisha wanawake wa UWT kuhusu Uchaguzi Mkuu mwaka huu.Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO.

Kikundi cha ngoma ya asili cha wakina mama mkoani Mbeya kikimtumbuiza Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) alipowasili (Agosti 28.2010) katika uwanja wa ndege wa Mkoani Mbeya katika muendelezo wa ziara zake za kuwahamasisha wanawake wa UWT kuhusu Uchaguzi Mkuu mwaka huu.Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

miss tanzania 2009 apongezwa na REDD'S katikua siku yake ya kuzaliwa


Meneja wa Kinywaji cha Redds Primaim Cold, Kabula Nshimo (kulia) akimkabidhi Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald keki ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa katika ukumbi wa Maasai Club mjini Arusha.
Miss Tanzania anaemaliza muda wake akikata keki ya sikukuu yake ya kuzaliwa huku akiwa amezunguwa na baadhi ya warembo wanaotarajia kuwania taji hilo mwaka huu.
Meneja wa kinywaji cha Redds Primaim Cold, Kabula Nshimo akimlisha keki Miss Tanzania anaemaliza muda wake katika sherehe ya kuzaliwa kwa mrembo huyo iliyofanyika katika ukumbi wa Maasai club mjini Arusha.
Miss Tanzania 2009 Miriam Gerald akiwalisha keki baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 katika hafla iliyoandalia na Kinywaji cha Redds na kuanyika katika ukumbi wa Maasai Club mjini Arusha.
Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Kaskazini Henry Tzamburakis (kulia) na Meneja wa Bia yaCol Redds Primim Cold, Kabula Nshimo (kulia) akimkabidhi Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald keki ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa katika ukumbi wa Maasai Club mjini Arusha.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA