
Dk Ally Mohamed Shein ameshinda Urais wa Zanzibar na amewapongeza wananchi wa Wazanzibar wote huku akimuomba mungu ampe hekima na busara ili kuiongoza vizuri Zanzibar na wananchi wake. Dk. Shein amemshukuru mpinzani wake Maalim Seif Sharif Hamad kwa kukubali matokeo hayo ya uchaguzi lakini pia amemshukuru kwa kutoka hotuba nzuri na yenye mwelekeo na uungwana kwa Wazanzibar wote huku akimsifu na kusema nuitashauriana vyema na kufanya kazi na maalim Seif Hamad kama Makamu wa Kwanza wa Rais Kwa moyo mmoja. Amesema uamuzi wa Asilimia 66 ya Wazanzibar ni uamuzi mzito kwani Zanzibar ni yetu wazanzibar wote na na tunatakiwa kuitumikia kwa pamoja ili kuendeleza nchi yetu nzuri ya Zanziba na lazima tuitumikie vizuri na kuienzi kama Wazanzibar wamoja. Dk Shein pia ameishukuru Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa kuandaa na kusimamia uchaguzi vizuri na kwa amani na kuhakikisha umefikia tamati kwa amani kabisa ambapo kwa sasa Serikali ya Mapinduzi Zanziba inakwenda kuundwa kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ikishirikisha vyama mbalimbali visiwani humo..
No comments:
Post a Comment