(Picha na Aron Msigwa)
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 31, 2010
KUTOKA JUKWAA LA SANAA,BASATA-FILAMU NA MAADILI YETU
FILAMU ZA KIBONGO MAADILI YAKE NI KIFO KWETU?
2. Kunakiri (copying) kazi za wasanii wa Nigeria na kutumia muziki (Sound Tracks) za wasanii wa muziki bila idhini yao.Katika haya wasanii wa Filamu wameshauriwa kuwa makini kwani sheria ya Hakimiliki inaweza kuwafunga.Kwa ujumla wasanii walishauriwa kuwekeza ubunifu binafsi na kubeba uhalisia wa sanaa yetu badala ya ilivyo sasa ambapo filamu zetu zimekuwa zikifanana fanana na zile za Nigeria.
3. Uchafu wa Filamu-Wadau wengi wamesema kwamba, filamu za kibongo zimekuwa na maadili mabovu yanayotokana uvaazi wa vichupi kwa wasanii wa kike, uoneshaji wa matendo ya faragha (mapenzi) mara kwa mara, script zenye kushabikia matendo maovu na yasiyofaa kwa jamii nk.Wadau walishauri Bodi ya Filamu, vituo vya TV na wasanii wenyewe kuhakikisha wanadhibiti filamu zisizo na maadili kwani zimekuwa zikitia aibu/kichefuchefu.Ilielezwa kwamba, baadhi ya filamu hazibebi uhusika wenye ufanano na maisha/maadili ya kitanzania.
JUMATATU IJAYO KWENYE JUKWAA LA SANAA
Mchango wa Kituo cha Utamaduni cha Kimataifa cha Ufaransa na Ubalozi wa Ufaransa Katika Ukuzaji wa Sanaa na Utamaduni Wetu.Tutakuwa na Wataalam kutoka Ubalozi wa Ufaransa.USIKOSEKANE.
Picha/Habari na Afisa Habari wa BASATA,
Alistide Kwizela
TENDWA KUTOA MAAMUZI PINGAMIZI LA CHADEMA BAADA YA SIKU TANO!
Msajili wa Vyama Vya Siasa Nchini John Tendwa amesema atatoa uamuzi wake dhidi ya malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA)kuhusu mgombea wa urais kupitia chama cha mapinduzi(CCM) baada ya siku tano.
Bwana Tendwa ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari hayo ofisini kwake jijini Dar es salaam baada ya kupokea malalamiko hayo rasmi leo.
‘’Nitatoa maamuzi hayo baada ya kupokea maelezo kutoka kwa mlalamikiwa dhidi ya malalamikaji yaliyowasilishwa,na nitatoa nakala ya maamuzi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi na Katibu Mkuu wa chama cha CHADEMA’’,Alisema Tendwa.
Akifafanua suala hilo Tendwa amesema baada ya maamuzi yake mlalamikaji na mlalamikiwa kama hawataridhika na uamuzi wake wanayo haki ya kwenda kutafuta haki yao kwenye vyombo vya sheria.
Aidha Msajili huyo Vyama ameongeza kuwa amepokea malalamiko hayo kwa mujibu wa sheria ya gharama za uchaguzi inachomkataza mgombea yeyote ambaye yeye mwenyewe, wakala wake au Chama chake kitafanya kitendo ambacho kimekatazwa kama ilivyoelekezwa kwenye sheria hiyo atakuwa au kitakuwa kimepoteza sifa za kushiriki mchakato wa uteuzi au uchaguzi.
Pingamizi hilo liliwasilishwa jana ofisi ya masajili huyo na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika wakimlalamikia Mgombea urais wa chama cha mapinduzi Jakaya Mrisho Kikwete kutumia madaraka yake kutoa ahadi kwenye kampeni na kutangaza nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi wakati wa kampeni.
WAREMBO VODACOM MISS TANZANIA WAELEZWA FAIDA ZINAZOTOKANA NA BIDHAA ZA VODACOM!!
Afisa Bidhaa wa Vodacom Tanzania Elihuruma Ngowi akiweka sawa picha kwenye Projekta wakati alipokuwa akiwasilisha mada kwa warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania juu ya umuhimu wa bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na kutolewa na kampuni ya Vodacom katika semina ambayo imefanyika kwenye kambi ya warembo hao Hoteli ya Giraffe Ocen View Mbezi Beach jijini Dar es salaam leo.
Meneja Mauzo wa M-PESA Jerome Munishi akitoa ufafanuzi juu ya huduma za hizo zinazotolewa na kampuni ya Vadacom Tanzania wakati wa semina ya warembo wanaoshiriki kwenye shindano la Vodacom Miss Tanzania katika Hoteli ya Giraffe Ocean View Mbezi Beach leo hii shindano hilo linatarajiwa kufanyika Septemba 11 mwaka huu. PRECISION AIR YAZINDUA NDEGE MPYA !!
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh.Mohammed Babu akikata utepe kama ishara ya kuzindua ndege mpya ya Precision ART 42- 500 iliyopewa jina la "Bukuoba" yenye uwezo wa kubeba abiria 48 ambayo itafanya safari zake kati ya Dar es salaam na Bukoba na kurudi Dar es salaam, ndege hiyo iliruka kutoka Dar es salaam kwenda Zanziar na kurudi kwa majaribio na inatarajia kuanza safari zake mwezi ujao, wanaoshuhudia katika picha kutoka kulia ni Jamal Hussein Afisa Mtendaji Mkuu Citi Bank, Allan Sharra Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air na kushoto ni Rubani wa Ndege hiyo Chohan Mbarouk
Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambaye alikuwa mgeni rasmi Mh. Mohamed Babu katikati akisubiri ndege itue ili kufanya uzinduzi rasmi kwa kukata utepe kulia ni Allan Sharra Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air kushoto ni Jamal Hussein Afisa Mtendaji Mkuu Citi Bank na mwisho kushoto ni Lucy Malu Meneja Mkazi Kenya Airways.
Hii ndiyo ndege mpya ya Precision Air ATR 42- 500 yenye uwezo wa kubeba abilia 48 itakayofanya safari zake kati ya Dar es salaam na Bukoba.
Meneja wa Uhusiano wa Kampuni ya SCANAD Barnabas Lugwisha akiwa na mmoja wa waalikwa katika ndege hiyo mpya ilifanya safari kati ya Zanzibar na Dar es salaam leo kwa ajili ya uzinduzi rasmi
Designers visiting the Textile Sector Development Unit
Dr. Bilal Aendelea na ziara ya kampeni masasi na nayumbu!!!
Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Bilal akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Nanyumbu baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Masasi leo
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab akimvisha skafu Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala leo mchana
Mgobea Mwenza wa urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Masasi, baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Newala, leo
Baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Newala Mkoa wa Mtwara, wakiwa katika magari kwenye msafara wa kumsindikiza Mgombea Mwenza wa nafsi ya urais, Dk Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akitoka Wilaya hiyo kuelekea Wilaya ya Masasi leo asubuhi
wananchi wa Kijiji cha Lukuledi Wilaya ya Masasi Mkoa wa Mtwara, waliojitokeza kumsikiliza mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia na kuwanadi wagombea Ubunge wa Jimbo la Lulindi,Bwanausi Dismas na Mariam Kasembe wa Jimbo la Masasi leotano Wa Marais Wastaafu Wafanyika Jijini Dar
(Picha na Aron Msigwa)
Aug 29, 2010
Chama cha NCCR Mageuzi chazindua ilani yake ya uchaguzi
Pichani ni mgombea urais kwa Chama cha NNCR Mageuzi, Hashim Rungwe akionyesha ilani ya uchaguzi ya chama hicho wakati wa uzinduzi wa kampeni ya chama hicho leo jijini Dar. CHAMA cha NCCR Mageuzi leo kimezindua ilani yake ya Uchaguzi huku kikitaja mambo 12 ambayo chama hicho kitaelekeza nguvu iwapo kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi.Wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa chama hicho taifa James Mbatia alisema chama chake kitazindua kampeni zake kitaifa Septemba 11 baada ya mfungo wa ramadhani ili kutowakwaza Waislam ambao wako kwenye mfungo wa mwezi mtukufu.“Ajenda yetu kuu itakuwa ni katiba, tumeainisha mambo yatakayokuwemo kwenye katiba hiyo, hili ndilo nataka wagombea wetu mlizungumzie kwa kina,” alisema Mbatia. VODACOM YAFUTURISHA PANGANI NA KUGAWA MISAADA YA CHAKULA KWENYE MADRASA!!

Mtoto Bwaga Abdallah akipokea mfuko wa sukari kutoka kwa Maafisa wa Vodacom Foundation Grace Lyon kulia na Mwamvua Mlangwa wa pili kutoka kulia huku akisaidiwa na Sheikh Mohamed Khalili kushoto kutoka Tanga mjini na Sheikh Khamis Rashid Mwakilishi wa Sheikh wa Pangani wa pili kutoka kushoto, katika msaada huo pia Vodacom Foundation iligawa Mchele, Maharage, mafuta ya kula pamoja na vifaa vya shule.
: wakazi wa mji wa Pangani waliojitokeza katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation wakisubiri muda ufike ili waweze kufuturu Vodacom Foundation pia iligawa misaada ya Mchele, Mafuta ya kula, maharage na vifaa vya shule kwa watoto wa Dadrasa mbalimbali na vituo vya watoto yatima mjini Pangani CUF wazindua kampeni zaao


Rais Kikwete Awasili Mkoani Mbeya
Dr.Bilal aendeleaa kuinadi ilani ya CCM mkoani mtwara
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Kijiji cha Ntiniko Wilaya ya Mtwara Vijijini Mkoa wa Mtwara.
Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal akipita katikati ya chipukizi baada ya kupokelewa katika mpaka wa Wilaya ya Mtwara Mjini na Tandahimba Mkoa wa Mtwara wakati akiwa kwenye ziara yake ya mikutano ya kampeni leo mchana.
Mgombea Mwenza wa nafasi ya urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Nanguruwe Wilaya ya Mtwara Vijijini baada ya kusimama eneo hilo wakati akielekea Kijiji cha Ntiniko katika mkutano wa kunadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo.
Wananchi wa Kijiji cha Nahyanga Wilaya ya Tandahimba Mkoa wa Mtwara, wakimsikiliza Mgombea mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal wakati wa mkutano wa kampeni.
Rais Kikwete apokelewa kwa shangwe sumbawanga na mpanda
Wanachi wa mji wa Sumbawanga wakiwa wamefurika ndani ya Uwanja wa Mandela kumsikiliza Rais Jakaya Kikwete wakati akiwahutubia.

















